Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 423 2021-06-15

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-

Mradi wa kusambaza umeme katika Jimbo la Kibaha Mjini unakwenda kwa kusuasua:-

Je, ni lini Mradi huo utakamilika ili Wananchi wa Kibaha Mjini waondokane na adha ya umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa kusambaza umeme kwa Wilaya ya Kibaha Mjini (Peri-Urban) ulianza mwezi Novemba, 2019. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo yanayonufaika na mradi huu ni pamoja na Pangani, Maili Moja, Picha ya Ndege na Sofu. Gharama ya Mradi ni shilingi bilioni 18.56.