Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Mbagala Kokoto hadi Kongowe wanaopisha ujenzi wa barabara ya Kilwa?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mchakato wa kuhakiki mali za wananchi pamoja na majedwali haya ya fidia ulianza toka mwaka 2018, je, wananchi wa Kokoto hadi Kongowe wanataka kujua wavumilie mpaka lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, ni nini hatma ya wananchi wa Mbagala Rangitatu eneo la Charambe hadi kule Mbande ambao wamewekewa mawe ya hifadhi ya barabara toka mwaka 2010 na bila kupewa maelezo yoyote? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chaurembo, Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza Mheshimiwa Mbunge wa Mbagala ambaye ni Meya Mstaafu wa Manispaa ya Temeke kilio chako kimesikika Mheshimiwa Mbunge na ndio maana Mheshimiwa Rais alitembelea katika eneo lako na ametoa maelekezo. Kiongozi Mkuu wa nchi akitembelea nchi hayo ni maelekezo sisi ni watekelezaji.

Mheshimiwa Spika, kilichofanyika ni kwamba ni fidia imefanyika, mkandarasi yupo pale site ataleta taarifa, watu wa TANROADS Mkoa wa Dar es salaam watapitia taarifa hiyo, tutafanya joint verification kwa maana ya Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Fedha na Valuer wa Serikali baada ya hapo wananchi wale watalipwa fidia. Maelekezo ni kwamba ujenzi hautaanza mpaka tuondoe vikwazo vya kulalamikiwa na wananchi baada ya kulipwa haki zao. Kwa hiyo, naomba wavute subira katika jambo hilo tunalifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili Mheshimiwa Mbunge anauliza habari ya mawe ambayo imewekwa pale katika road reserve ya Mbande kwenda Msongola mpaka Mvuti. Ni kweli kwamba wananchi baadhi walilipwa wakati huo, lakini tumekubaliana kwamba tukianza upanuzi wa barabara hiyo, yule mwananchi ambaye anafikiwa kwa wakati huo atakuwa analipwa fidia yake, hayo ndio majibu ya Serikali, ahsante sana.