Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 49 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 408 2021-06-10

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Mbagala Kokoto hadi Kongowe wanaopisha ujenzi wa barabara ya Kilwa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge wa Mbagala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara Ujenzi na Uchukuzi ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi wa barabara kwa lengo la kushughulikia tatizo sugu la msongamano wa magari, hususan katika barabara kuu za Jiji la Dar es Salaam ikiwemo barabara ya Kilwa kuanzia Mbagala Rangitatu mpaka Kongowe yenye urefu wa kilometa 3.8. Utekelezaji wa mpango huu unahusisha upanuzi wa barabara kutoka njia mbili kuwa njia nne pamoja na ujenzi wa Daraja la Mzinga.

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha ujenzi huo unafanyika bila vikwazo, Wizara kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha hatua za awali za kupitia jedwali la fidia na kuhakiki mali za wananchi wanaostahili kulipwa fidia. Aidha, zoezi hili liliwahusisha pia viongozi wa Serikali za Mitaa husika ili kuhakikisha wananchi wote wanaostahili kulipwa fidia wanalipwa stahili zao kwa mujibu wa sheria zilizopo. Hivyo wananchi wa Mbagala eneo la Kokoto hadi Kongowe wanaombwa kuwa wavumilivu wakati zoezi la kuhakiki taarifa za fidia linaendelea. Mara uhakiki utakapokamilika wahusika wote watalipwa fidia kulingana na sheria, kanuni na taratibu zilizopo, ahsante.