Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je lini Serikali itaajiri walimu wa masomo ya sayansi katika Shule za Sekondari za Halmashauri ya Mji Mbulu ili wanafunzi wapate ujuzi wa masuala ya sayansi?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana; pamoja na majibu mazuri ya Serikali, majibu ambayo yanaeleza ni walimu kumi tu wa sayansi walioajiriwa kwa muda wa miaka mitano hali inayopelekea wanafunzi wengi wa Jimbo la Mbulu Mji na maeneo mengine nchini kushindwa kufanya mazoezi ya sayansi, na kwa kuwa tatizo hili limewagharimu wananchi kwa muda mrefu kwa ajili ya kuwachangia walimu wa kujitolea katika shule za Halmashauri ya Mji wa Mbulu.

Nini kauli ya Serikali ya kutusaidia walau tatizo hili linapungua katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu pamoja na maeneo mengine nchini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa sasa tupo kwenye mchakato wa ajira na majibu ya awali nilipofuatilia Wizarani walikuwa wamesema tuna walimu wengi wa sayansi na tatizo hili limewagharimu wanafunzi hao wasifanye vizuri.

Je, Serikali ipo tayari sasa kutoa nafasi pekee ya kuondoa walau kiasi kikubwa cha upungufu wa walimu kwa shule za sekondari katika Jimbo la Mbulu Mji? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zacharia Paul Issaay, Mbunge wa Mbulu Mji kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza alikuwa nataka kujua kauli ya Serikali ya kupunguza tatizo la walimu wa sayansi hususan katika eneo lake lakini na maeneo mengine nchini; ni kama nilivyoeleza katika jibu la msingi kwamba Serikali itaendelea kuajiri walimu na tutaendelea kuangalia kada mbalimbali hususan kada za walimu wa sayansi pamoja na wataalam na mafundi sanifu wa maabara ili tuweze kuwasaidia.

Kwa hiyo, miongoni mwa vigezo ambavyo tumevizingatia sana ukiacha vile vigezo vya awali ambavyo tulivitaja ikiwemo watu kukaa muda mrefu ambao hawajapata ajira, lakini miongoni mwa vigezo ambavyo tunavitumia sasa hivi ni pamoja na ku-consider walimu wa sayansi katika ajira hizi ambazo tutazitoa hivi karibuni.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nimtoe wasiwasi tu kwamba Serikali tutaendelea kuwapanga katika maeneo yote ikiwemo katika eneo lako la Mbulu Mji. Kwa hiyo, hilo niahidi kwa Wabunge wote kwamba tutazingatia Majimbo yote katika kipindi hiki kuwaletea walimu wa sayansi lakini hatutawaacha na walimu wa arts ambao wamesoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili ni kwamba alitaka tu kujua ni namna gani tunawasaidia kuwatoa. Jukumu kubwa ni kwamba Serikali itaendelea kuajiri kulingana na upatikanaji wa fedha na kadri tutakavyoajiri ndivyo ambavyo tutaendelea kuwapanga, ahsante sana. (Makofi)

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Je lini Serikali itaajiri walimu wa masomo ya sayansi katika Shule za Sekondari za Halmashauri ya Mji Mbulu ili wanafunzi wapate ujuzi wa masuala ya sayansi?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hali iliyopo Halmashauri ya Mji wa Mbulu ya ukosefu wa walimu wa sayansi inafanana kabisa na hali ya Halmashauri zote za Mkoa wa Pwani kuwa na uhaba wa walimu wa sayansi.

Je, ni lini sasa Serikali itatupatia walimu hawa wa sayansi ili kuweza kukidhi mahitaji? Ahsante. (Makofi)

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Naibu Waziri Mheshimiwa Silinde kwa majibu mazuri, lakini nimshukuru sana Mheshimiwa Hawa Mchafu kutaka kujua ni lini Serikali itapeleka walimu wa sayansi katika shule za sekondari za Mkoa wa Pwani.

Mheshimiwa Spika, kama ulivyosema, tunakiri tunayo changamoto ya uhaba wa walimu wa sayansi na uchambuzi ambao tumeufanya ndani ya miezi mitatu kuna shule takribani 1,000 za sekondari wanafunzi wetu hawajawahi kukutana na mwalimu wa physics face to face, lakini tuna shule takribani 400 watoto wetu wa sekondari hawajawahi kumuona mwalimu wa hesabu akiingia darasani.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tatizo hili tumeliona na tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutupa kibali cha kuajiri walimu katika mwaka huu wa fedha wa 2020/2021. (Makofi)

Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wabunge tunakamilisha uchambuzi wa maombi ya walimu ambao wameomba nafasi hizi za ajira tulizozitoa na kipaumbele kama tulivyosema ni kutatua changamoto hii ya walimu wa sayansi hususan pia katika masomo ya hesabu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niongeze, sambamba na kuendelea kuomba kibali cha ajira kutoka kwa wenzetu Ofisi ya Rais - Utumishi tumeona ipo fursa ya kutumia maendeleo ya Information Communication and Technology (ICT) ili pia kuwawezesha wanafunzi wetu kupata masomo au walimu wa sayansi na hesabu kupitia mtandao.

Kwa hiyo, hili ni jambo ambalo tumeliona, tutaweka walimu wazuri watarekodi mada zote muhimu halafu wanafunzi wetu watakuwa pia wanaweza kusoma masomo ya sayansi kwa kutumia njia ya mtandano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. (Makofi)