Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 49 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 406 2021-06-10

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:-

Je lini Serikali itaajiri walimu wa masomo ya sayansi katika Shule za Sekondari za Halmashauri ya Mji Mbulu ili wanafunzi wapate ujuzi wa masuala ya sayansi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paul Issaay , Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017 hadi 2019/2020 Serikali imeajiri na kuwapanga walimu 17 wa sayansi na hisabati na mafundi sanifu wa maabara wawili katika Halmashauri ya Mji Mbulu kati ya walimu 10,418 wa Sekondari na mafundi sanifu maabara 397 walioajriwa katika kipindi hicho.

Aidha, Serikali inaendelea kuratibu zoezi la kuajiri walimu 6,949 kwa nafasi za ajira zilizotangazwa mwezi Mei, 2021 ambao watapangwa kwenye shule mbalimbali zikiwemo na shule za Halmashauri ya Mji Mbulu.