Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Kintiku -Lusilile?

Supplementary Question 1

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mradi wa Maji Kintinku - Lusilile, ulianza kutekelezwa toka mwaka 2013 na ulikadiriwa kutumia kiasi cha shilingi bilioni tisa, na Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba endapo mradi huu ungekamilika ungeweza kuwanufaisha wananchi zaidi ya 55,000 wa vijiji 10 vikiwemo vya Mvumi, Lusilile, Ngwasa na Mwiboo.

Mheshimiwa Naibu Spika, toka nimeingia ndani ya Bunge hili nimekuwa nikiulizia mradi huu na kuupigia kelele; je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kutenga fedha za kutosha ili mradi huu ukamilike na uweze kuwanufaisha wananchi wa Jimbo la Manyoni Mashariki?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa Serikali inatumia fedha nyingi za walipa kodi, lakini ipo miradi ambayo imekamilika ya Mtama A na Mtama B; na miradi hii haitowi maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha miradi hii inatoa maji na wananchi wanapata huduma hii ya maji? Nakushukuru sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aysharose kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mradi ulianza mwaka huo alioutaja 2013 lakini jitihada nyingi zimeshafanyika baada ya RUWASA kuanzishwa na amini Mheshimiwa Aysharose kwa namna ya ufuatiliaji wako wa mara kwa mara na hata umeomba kuweza kwenda na mimi kule na nimeshakuahidi tutakwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nikupe taarifa tu kwamba kwa kipindi hiki toka mwezi Mei mpaka dakika hii ninavyoongea huu mradi umeshakamilika zaidi ya asilimia 95, bado sehemu ndogo tu mradi huu unaenda kukamilika na ni fedha nyingi tayari zimeshaelekezwa huko na sehemu iliyobaki fedha pia itapelekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miradi ambayo imekamilika suala la Wizara ni kuona kwamba maji yanatoka mara baada ya miradi hii kukamilika. Hivyo, kwa miradi yote ambayo imeshakamilika nipende kuendelea kuwaagiza wataalamu wetu maeneo yote, miradi ambayo imekamilika wahakikishe wanaanza kupekeka maji katika vituo vya kuchotea maji ili wananchi waweze kunufaika na fedha ambazo Serikali imepeleka katika maeneo yote, hivyo na wewe katika eneo lako la Singida Mashariki pia maji yataanza kutoka katika maeneo yote miradi ilipikamika.