Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 48 Water and Irrigation Wizara ya Maji 401 2021-06-09

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Kintiku -Lusilile?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aysharose Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Kintinku -Lusilile ni mradi mkubwa ambao unatekelezwa kwa awamu nne na hadi mwezi Mei, 2021 utekelezaji wa awamu ya kwanza imekamilika ambayo ilihusisha ujenzi wa tenki la kukusanya maji la lita 300,000, ujenzi wa nyumba ya mtambo wa kusukuma maji na kufunga mitambo ya kusukuma maji, ujenzi wa tanki la kuhifadhi maji lita milioni mbili na ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilometa 1.2. Aidha, utekelezaji wa awamu ya pili unaohusisha ulazaji wa mabomba ya usambazaji umbali wa kilometa 1.3 unaendelea na unatarajiwa vijiji vitatu vya Chikuyu, Mwiboo na Mbwasa ambavyo vina jumla ya wakazi wapatao 6,020 vitaanza kunufaika na huduma ya maji kabla ya mwezi Julai, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huu unatarajia kukamilika katika mwaka wa fedha 2021/2022 na utahudumia wakazi zaidi ya 55,000 wa vijiji 11.