Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa uwanja mpya wa ndege katika Mji wa Njombe utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyatoa, naomba niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Njombe ni moja katika mikoa mitano bora ambayo imefikia kiwango cha uchumi wa kati kwa watu wake, mkoa huu ni moja kati ya Halmshauri 10 bora kwa makusanyo zinazizidi hata Manispaa zaidi ya 10 katika nchi hii. Mkoa wa Njombe ni mkoa ambao una miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo parachichi pamoja na Liganga.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa swali langu; hivi ni kigezo gani kinachotumika maana wasiwasi wetu hata katika viwanja 11 tunaweza tukawa wa mwisho kwa sababu sioni ni vigezo gani, ukienda kwa niliyoyasema Mkoa wa Njombe unatakiwa uwe mkoa wa mwanzo kupata uwanja wa ndege? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tunatambua mchango mkubwa wa kiuchumi kutoka Mkoa wa Njombe kwa ujumla wake pamoja na Njombe Mjini. Lakini vilevile uwezo wa Serikali siyo mkubwa kiasi hicho kujenga viwanja hivi vyote 11 kwa wakati mmoja. Safari ni atua upembuzi yakinifu umefanyika sasa tunajua gharama ya kujenga uwanja wa ndege wa Njombe ni gharama kiasi gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukweli ni kwamba unaangalia, ameuliza vigezo kwa mfano, pale Iringa mjini kuelekea Mkoa wa Iringa karibu kabisa na Makambako na Mkoa wa Njombe, sasa hivi tunazungumza mkandarasi yuko site anaendelea kufanya kazi ya kumaliza runway ili ndege aina zote ziweze kutua eneo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa wakati ambao Serikali inaendelea kupata fedha kutoka mapato ya ndani na washirika wengine wa kimaendeleo, watu wanaotaka kwenda Njombe wanaweza kutumia alternative kutumia uwanja Iringa baada ya kuwa umekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali yake ni njema tungependa kila Mkoa uwe na uwanja wa ndege na Waheshimiwa Wabunge wakitoka hapa baada ya Bunge kuahirishwa wangependa kutoa katika mikoa yao, lakini kwa kuwa fedha nyingi kiasi hicho tuvumiliane tupeane muda kazi hii itakamilika, ahsante sana.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa uwanja mpya wa ndege katika Mji wa Njombe utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. MKUNDI M. JOSEPH: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, pale Ukerewe tuna kiwanja kidogo cha ndege na kama kitaboreshwa kitasaidia sana kuchochea vivutio vya utalii na kuvitangaza vilivyopo Ukerewe, lakini na kuchochea uchumi wa Ukerewe na wananchi wa ukanda ule kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, nini mkakati wa Serikali kukiboresha kiwanja kidogo cha ndege kilichopo kwenye visiwa vya Ukerewe? Nashukuru.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Mkundi Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Ukerewe ni eneo la kisiwa na kwa sababu hiyo usafiri pekee ambao unatumika ni aidha, kutumia anga au kupita majini. Mheshimiwa Mbunge nampongeza kwa kuombea wananchi wake wameshapata kivuko inafanya kazi katika eneo lile na hili wazo tunaomba tulipokee.

Mheshimiwa Naibu Spika, nia ya Serikali ni ya kuboresha viwanja vyetu vya ndege na hasa eneo kama Ukerewe ambalo kuna mambo ya kiutalii, wageni wanaweza wakatua pale, kuna shida ya kiusafiri, hili tunalipokea tunalifanyia kazi, tukipata fedha za kutosha Mheshimiwa Mbunge nakuhakikishia eneo lako litaboreshwa zaidi ya hapo lilipo ahsante sana.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa uwanja mpya wa ndege katika Mji wa Njombe utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa nafasi naomba kufahamu Serikali lini itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege wa Manyara ili kurahisisha usafiri na usafirishaji kwa wakulima wafugaji na wafanyabiashara wa Mkoa wa Manyara?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge la nyongeza juu ya uwanja wa Manyara kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali nililoulizwa na Mheshimiwa Phillip Mwanyika kutoka Njombe Mjini, nimesema kwenye jibu la msingi kwamba viwanja 11 vimefanyiwa tathmini na upembuzi yakinifu, tunajua gharama zilizopo, uwanja wake Mheshimiwa Mbunge na Mkoa wa Manyara kwa ujumla upo kwenye mpango huu, tunatafuta fedha na zikipatikana wakati wowote uwanja wake wa Manyara, pamoja na viwanja vingine 11 ambavyo nimevitaja hapa vitajengwa ili ndege iweze kutoa huduma katika mikoa hiyo. Ahsante.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa uwanja mpya wa ndege katika Mji wa Njombe utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipatia nafasi hii. Mkoa wa Kagera kwa muda mrefu kumekuwa na uwanja wetu wa ndege wa kimataifa Omukajunguti.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua ni lini uwanja huu wa Omukajunguzi utajengwa? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa kipaumbele cha Serikali ni kuboresha uwanja wa ndege wa Bukoba, uwanja wa kimataifa na kwenye bajeti ya mwaka ambayo imepitishwa mwezi uliopita tarehe 27 na tarehe 28. Uwanja ule tunatarajia kujenga jengo la abiria maarufu kama VIP, lakini pia na kuongeza runway ili ndege nyingi kubwa ziweze kutoa katika eneo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka huu wa fedha Mheshimiwa Mbunge watu wa Bukoba na maeneo ya jirani muwe na Amani tunajenga uwanja ule jengo la abiria maarufu lakini pia na run way utapata usafiri.