Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 48 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 400 2021-06-09

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa uwanja mpya wa ndege katika Mji wa Njombe utaanza?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): alijibu

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimwa Deodatus Phillip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanja cha ndege cha Njombe ni miongoni mwa viwanja 11 vya ndege vilivyofanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ufadhili wa Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Transport Sector Support Project (TSSP). Viwanja hivyo 11 ni pamoja na Lake Manyara, Musoma, Songea, Kilwa Masoko, Tanga, Iringa, Lindi, Moshi, Singida, Njombe na Simiyu.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hatua ya awali ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika, Serikali imejipanga kuanza ujenzi kwa hatua mbalimbali kwa awamu kwa kutumia fedha za ndani, lakini kutokana na ukweli kwamba gharama za ujenzi wa viwanja hivyo ni kubwa ukilinganisha na bajeti inayotolewa kila mwaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia bajeti, Serikali kupitia TANROADS imejipanga kuanza na ujenzi wa viwanja vya ndege vya Iringa na Songea. Ujenzi wa viwanja vilivyobaki kikiwemo cha Njombe utaanza mara Serikali itakapopata fedha. Aidha, kwa sasa Serikali inaendelea kuwasiliana na washirika wa maendeleo ili kuweza kupata fedha za kujenga viwanja hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maelezo hayo hapo juu, namuomba Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika pamoja na wananchi wa Njombe Mjini waendelee kuvuta subira kwani Serikali ina nia ya dhati ya kujenga kiwanja hicho.