Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha kilimo cha mkataba kwa njia ya outgrower scheme ili kupanua wigo wa upatikanaji wa soko kwa wakulima wadogo wadogo?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri sana yanayotia moyo ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa kilimo cha mkataba ni kilimo ambacho kinahitaji mahitaji muhimu sana na mengi ili kifanikiwe mojawapo kubwa ni mbegu bora. Je, Wizara imejipangaje kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Singida na hasa Mkalama wanapata mbegu bora na kwa bei rahisi?

Swali la pili, kwa kuwa viwanda vingi vya alizeti Mkoa wa Singida vinafanyakazi kwa miezi mitatu tu kwa sababu ya ukosefu wa mbegu, Wizara imejipangaje kuhakikisha kwamba tatizo hili linatatuliwa Serikali inapata mapato na inatatua tatizo kubwa la mafuta ya mboga nchini? Ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Francis Isack kama ifuatavyo:-

Kwanza nitumie Bunge lako Tukufu kuwaalika Wabunge wa maeneo ya Singida, Dodoma na Manyara katika mkutano utakaoongozwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu siku ya tarehe 13 Juni unaohusiana na suala la alizeti na mazao ya mafuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua tunayoichukua ya kwanza Wizara sasa hivi inafanya tathmini ya mahitaji ya mbegu zitakazochakatwa na viwanda ili kuweza kuondoa gap ya mafuta. Hatua ya pili tuta-subsidize mbegu kupitia maviwanda badala ya mbegu ya high sun kununuliwa kwa shilingi 30,000 Serikali inafanya tathmini sasa hivi tuta-subsidize kwa kiwango kisichopungua asilimia 50 ya bei hiyo ili wakulima waweze kupata mbegu hizi kwa bei rahisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hatua ya tatu tunayochukua gap mahitaji yetu ya mbegu kwa ajili ya kuzalisha alizeti zitakazotosheleza viwanda vyote kwa msimu wa mwaka mzima ni metric tans 3,900 na sisi kama Serikali uwezo wetu wa uzalishaji wa ndani ni metric tans zisizozidi 700. Wizara sasa hivi inafanya mchakato wa kuagiza mbegu metric tans 3,000 ambazo zitakuwa subsidize na hizo tutazigawa kwa wakulima kwa bei rahisi ili viwanda viweze kupata alizeti ya kutosha katika msimu ujao.

Kwa hiyo, kwa misimu ya miaka miwili tutaagiza gap na msimu wa tatu kwa fedha mlizotupitishia mwaka huu katika bajeti kwa ajili ya ASA tutakuwa na uwezo wa kuzalisha mbegu zote za alizeti ndani ya nchi yetu na hatutokuwa na gap. (Makofi)

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha kilimo cha mkataba kwa njia ya outgrower scheme ili kupanua wigo wa upatikanaji wa soko kwa wakulima wadogo wadogo?

Supplementary Question 2

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, msimu wa zao la pamba umefunguliwa tarehe 10 Mei na mategemeo ya wakulima ni kwamba wanapokwenda kuuza zao lao waweze kulipwa fedha zao.

Je, Wizara ya Kilimo imejipanga vipi kuhakikisha kwamba inawasimamia wenye viwanda wasiende kukopa zao la wakulima?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Magoto, Mbunge wa Bunda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tumetoa waraka kupitia Bodi ya Pamba, nunuzi yoyote anapochukua pama katika chama cha msingi ni lazima mkulima awe amelipwa ndani ya muda usiozidi saa 48 na mnunuzi yeyote atakayekwenda kinyume na hili tutamfutia leseni na kumuondoa kwenye database ya ununuzi wa pamba, hakuna kukopa pamba ya mkulima, hili ni la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili tumetoa bei dira ambayo wakulima ni lazima walipwe kiwango kisicho pungua bei hiyo, lakini wakati huo huo ushindani unaendelea, bei dira tuliosema Wizara ya Kilimo haitakiwi kupungua shilingi 1,050 bei ya chini ingawa bei inayoendelea sasa hivi ushindani umefika mpaka shilingi 1,100/1,150 na kila mnunuzi aweke pango la bei yake kwenye AMCOS ili mkulima anapopima pamba yake ajuwe bei ya siku hiyo ni shilingi ngapi na viongozi wa AMCOS wahakikishe wanamlipa bei iliyoko sokoni siku hiyo.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha kilimo cha mkataba kwa njia ya outgrower scheme ili kupanua wigo wa upatikanaji wa soko kwa wakulima wadogo wadogo?

Supplementary Question 3

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Lushoto ina wakulima wadogo wadogo wa njegere na zao hili linapendwa sana nchi za nje; je, Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea mitaji wakulima hawa hasa wakulima wa Kijiji cha Bombo, Ubiri, Jogoi, Ngare na maeneo mengine ya Wilaya ya Lushoto? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shekilindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nitumie Bunge lako Tukufu, pamoja na kujenga mazingira mazuri ya mabenki kuendelea kuwapatia mikopo wakulima niziombe Halmashauri za nchi yetu mnatenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kukopesha wajasiriamali, kilimo ni biashara, wajasiriamali siyo mama ntilie tu wala siyo madereva wa bodaboda. Niziombe Halmashauri pelekeni asilimia 10 mnazotenga katika Halmashauri zenu kwenye sekta ya Kilimo return on investment is 100% na wala hakuna defaulters kwenye kilimo unless kuna risk. Tuache kukopesha wachuuzi twendeni kwenye uzalishaji. (Makofi)