Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 48 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 399 2021-06-09

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha kilimo cha mkataba kwa njia ya outgrower scheme ili kupanua wigo wa upatikanaji wa soko kwa wakulima wadogo wadogo?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo cha mkataba kinawezesha wakulima kuwa na soko la uhakika na wanunuzi kununua kuwa na mazao yenye ubora kulingana na mahitaji. Aidha, kilimo cha mkataba kinachangia kutatua changamoto za upatikanaji wa pembejeo za kilimo na kuimarisha upatikanaji wa mitaji kutokana na makubaliano baina ya mkulima, taasisi za fedha na wanunuzi wa mazao husika kulingana na mahitaji ya soko.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia msimu wa kilimo wa mwaka 2021/2022 kilimo cha alizeti kitakuwa cha mkataba na mpaka sasa Wizara imewasiliana na Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na Miji ili kusimamia kilimo cha mkataba. Kilimo cha mkataba kimeleta matokeo mazuri katika zao la ngano katika Mikoa ya Manyara, Kilimanjaro na Arusha.

Aidha, tayari Serikali imekutana na makampuni ya Pyxus Tanzania Agriculture Limited, Mount Meru, Mwenge Sunflowers na makampuni mengine yanayozalisha mazao ya alizeti kama Jackma CO. Ltd. yamefanya vizuri katika mikoa ya Manyara katika kilimo cha mkataba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutumia kilimo cha mkataba Wizara kwa kushirikiana na Sekta binafsi inaendelea kuhamasisha wakulima kushiriki katika kilimo cha mkataba ambacho kimeonesha mwelekeo mpya katika kuhakikisha masoko ya uhakika, bei nzuri na viwango bora vya mazao ya kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inatekeleza haya kwa kuzingatia Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 na maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa sekta ya kilimo ijitegemee.