Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Magu - Bukwimba - Ngudu - Hungumalwa itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pia nishukuru kwa majibu ya utangulizi, lakini naomba tu kuiambia Serikali kwamba barabara hii ni muhimu sana kwa ajili ya uchumi pamoja na kijamii. Pia niseme barabara hii ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne na wakati barabara hii inaahidiwa na Rais wa Awamu ya Nne, Rais wa sasa Dkt. John Pombe Magufuli alikuwepo. Sasa hili suala la upembuzi yakinifu, ni lini hasa kwa sababu swali hapa la msingi, ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami kwa kuzingatia kwamba hii ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna nilivyomwelewa, anasisitiza tu kwamba hii kazi ya upembuzi yakinifu ikamilike haraka ili ahadi ya Marais wetu, Rais wa Awamu ya Nne na Rais wa Awamu ya Tano wakati alipokuwa Waziri wa Wizara ya Ujenzi itekelezwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumthibitishia kwamba Wizara yetu itatekeleza ahadi hiyo kikamilifu.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Magu - Bukwimba - Ngudu - Hungumalwa itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa ujenzi wa barabara ni kichocheo kikubwa kwa shughuli za kiuchumi.
Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Tanga - Pangani - Saadani utaanza?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge, barabara hii ili tuweze kuitendea haki, tuwasiliane Wizarani ili wataalam nao watoe mchango wao ili tunapotoa tarehe ya lini itaanza iwe taarifa sahihi. (Makofi)