Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 2 | sitting 3 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 35 | 2016-01-28 |
Name
Richard Mganga Ndassa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sumve
Primary Question
MHE. RICHARD M. NDASSA aliuliza:-
Je, ni lini barabara ya Magu - Bukwimba - Ngudu - Hungumalwa itajengwa kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kuchukua nafasi hii kujibu swali la Mheshimiwa Richard Mganga Ndassa, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2010/2011 na 2011/2012, Wizara kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) ilitenga jumla ya shilingi milioni 1200 ambazo zilitumika kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Magu - Ngudu - Jojiro sehemu ya Ngudu Mjini yenye urefu wa kilometa 1.9
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2014/2015 na 2015/2016, Serikali ilitenga jumla ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 70 na taratibu za kumtafuta Mhandisi Mshauri zinaendelea. Baada ya kukamilika kwa usanifu na gharama za mradi huo kujulikana, Serikali itatafuta fedha za kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved