Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya mipaka kati ya Vijiji vya Mwanholo na Nyenze dhidi ya Mwekezaji na Mchimbaji Madini Eli Hilal Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; katika majibu haya, inaonesha kwamba maelekezo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa yametolewa tangu mwezi Februari, lakini unaweza ukaona ni miezi takribani minne lakini hakuna hatua ya majibu ama ya utekelezaji juu ya suala hili la mgogoro.

Je, Serikali ipo tayari kuhakikisha kwamba inaweka msukumo wa haraka ili mradi utatuzi huu uweze kufanyika haraka na wananchi waendelee na majukumu yao kama kawaida? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kuambatana na mimi ili kwa pamoja tuweze kwenda kuona maeneo ya mipaka na kuona njia bora ya kuweza kutatua tatizo hili kwa haraka? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Butondo kwamba mwezi Februari ni kipindi ambacho Kamati Maalum ya Wataalam ilipoundwa na Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kufanya tathmini na kuangalia chanzo na pia kupendekeza njia muafaka za kwenda kutatua changamoto ya mgogoro kati ya vijiji hivi viwili na mwekezaji. Walipewa miezi mitatu, wameshakamilisha mwezi Mei mwaka huu, 2021, kwa hiyo, hivi sasa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ipo katika hatua za kufanya tathmini na kutoa maelekezo ambayo yatakuwa yanaleta tija katika mgogoro huu. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba Serikali imelichukulia kwa uzito sana suala hili na inalipeleka kwa haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali kwa maana Ofisi ya Rais, TAMISEMI na mimi nipo tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge mpaka kule Jimboni Kishapu ili tuweze kuona maeneo hayo na pia kwa kushirikiana na uongozi uliopo tuweze kupata suluhu ya mgogoro huo. Nakushukuru sana.