Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa wananchi maeneo ya Hifadhi ya Kitulo ambayo hayatumiki ili wayatumie kulisha mifugo yao hususani eneo la Kwipanya?

Supplementary Question 1

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyogeza.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kwamba mipaka ya Hifadhi hii ya Kitulo ilikosewa kwa sababu walikuwa wanatumia vijana ambao walikuwa wakibeba zile zege au beacon na kwa kuwa zilikuwa ni nzito sana walikuwa wanatua mahala ambapo siyo mipaka. Maana wanapotua ndiyo hapo hapo wanafanya mpaka na kusababisha baadhi ya taasisi kama shule mbili pamoja na jamii/familia/kaya kuwa ndani ya hifadhi. Je Serikali iko tayari sasa kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi kwenda kurekebisha mipaka hii ili iwe na uhalisia ama original yake ilivyokuwa inatakiwa iwe? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Hifadhi ya Kitulo inajulikana kama bustani ya Mungu kwa sababu ina maua ambayo yanachua na ni hifadhi pekee kwa Afrika ambayo ina maua mazuri sana na kwa bahati mbaya sana haijatangazwa ipasavyo. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba Hifadhi hii ya Kitulo inatangazwa ili ijulikane kama zilivyo hifadhi nyingine? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Atupele Mwakibete, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu mipaka kwamba ilikosewa, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaongozana na yeye pamoja na watalaam wa Wizara ya Maliasili na Utalii lakini pia nitaomba wataalam wanaotoka katika Wizara ya Ardhi ili twende kuangalia. Pale ambapo itathibitika kwamba mipaka hii ilikosewa basi tutaweza kuirekebisha.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala hili linalohusiana na utalii, nimhakikishie tu Mbunge kwamba bajeti ya mwaka 2021/2022 imezingatia maeneo muhimu likiwemo eneo hili la Hifadhi ya Kitulo kuitangaza kwa nguvu zote na ukizingatia kwamba hifadhi hii ni ya kipekee hapa nchini. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba hifadhi hii itatangazwa kwa nguvu zote ili watalii waweze kufika katika hifadhi hiyo.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii. Kutokana na changamoto zinazojitokeza katika tafsiri hasa ya mipaka kwenye maeneo ya wananchi pamoja na hifadhi, Wizara ya Ardhi kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii tutaweka utaratibu ambao tunakwenda kupitia mpaka mmoja baada ya mwingine ikiwemo hata ile ya Kazimzumbwe ambayo imekuwa na shida nyingi. Kwa hiyo, tutaifanya kazi hiyo tukishirikisha na wananchi wa maeneo husika ili tuweze kupata tafsiri sahihi tujue ni kweli mipaka imehama au namna gani kwa sababu kumekuwa na kelele nyingi kuhusiana na maeneo ya hifadhi na wananchi. (Makofi)