Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 43 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 363 2021-06-03

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa wananchi maeneo ya Hifadhi ya Kitulo ambayo hayatumiki ili wayatumie kulisha mifugo yao hususani eneo la Kwipanya?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Atupele Mwakibete, Mbunge wa Busokelo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Taifa Kitulo ilianzishwa kwa GN. Na.279 ya mwaka 2005. Maeneo yote yaliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa Kitulo likiwemo eneo la Kwipanya yamehifadhiwa kisheria kulingana na umuhimu wake kiikolojia, kijamii, kitamaduni na kiuchumi. Miongoni mwa sababu zilizopelekea Serikali kuanzisha Hifadhi hii ni pamoja na:-

(i) Kuhifadhi vyanzo vya maji ambavyo vinatoa maji yanayoenda kwenye Bonde la Ziwa Nyasa na Bonde la Mto Rufiji ambapo kwa sasa maji hayo yanachangia kwenye miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Kufua Umeme wa Maji uliopo katika Bwawa la Julius Nyerere pamoja na Bwawa la kufua umeme wa maji la Mtera;

(ii) Eneo hili linahifadhi uoto adimu wa asili wa misitu na maua uliopo katika eneo husika;

(iii) Kutunza makazi ya wanyama adimu duniani kama vile Kipunji na Minde; na

(iv) Pamoja na kuhifadhi mandhari ya asili ya milima kwa ajili ya shughuli za utalii.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuhifadhi eneo hili la Taifa la Kitulo kutokana na umuhimu wake. Ahsante.