Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaainisha mpaka kati ya Wilaya ya Mkalama na Hanang’ eneo la Singa na Limbadau ili kuondoa taaruki kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba jina langu ni Francis Isack Mtinga, sio Mtenga, Mtenga ni Wachaga, Mtinga ni Wanyiramba.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa maelezo mazuri ya waziri ya kukiri mgogoro lakini nakiri sijaridhishwa kabisa na jibu walilolitoa. Na hivyo nitauliza swali moja tu la nyongeza ili nitoe na maelezo kidogo.

Mheshimiwa Spika, mpaka huu ni wa mkoa; mpaka kati ya Hanang’ na Mbulu na Wilaya ya Mkalama ni mpaka wa Mkoa wa Manyara na Mkoa wa Singida na amekiri kwamba tatizo hili ni la muda mrefu sana lakini majibu aliyoyatoa kwamba ni kupima, kupima hakutatui tatizo la mgogoro. Na tatizo hili limekuwa kubwa sasa kule Kijiji cha Eshkeshi, Wilaya ya Mbulu wameingia kilometa mbili katika Kijiji cha Ulamoto kule...

SPIKA: Uliza swali!

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, naomba Waziri aniambie kwamba lini tutakwenda naye akafanye mkutano na wataalam kwa vijiji hivi ili kutambua mipaka ili kuondoa mgogoro huu na wananchi wafanye kazi za utawala vizuri, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Isaack.

Mheshimiwa Spika, suala la kutambua migogoro katika mpaka sio kufanya mikutano tu, kinachotakiwa pale ni kwenda na GN zinazohusika na kufanya tafsiri ya GN kuangalia zile coordinates katika yale maeneo. Naomba nimuhidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tukimaliza tutampa wapima watakwenda wakiwa na zile GN zinazotaja mipaka ya Wilaya zote mbili ili waweze kutambua na kuweza kubainisha mipaka. (Makofi)