Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 352 2021-06-02

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je ni lini Serikali itaainisha mpaka kati ya Wilaya ya Mkalama na Hanang’ eneo la Singa na Limbadau ili kuondoa taaruki kwa wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa kuna mgogoro wa mipaka ya Vijiji kati ya Wilaya za Mkalama na Hanang ambao umekuwepo kwa muda mrefu licha ya jitihada mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali ikwemo vikao vya ujirani mwema baina ya wahusika wa mgogoro, Serikali ilitekeleza uwekaji wa alama za mipaka iliyotangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 266 la tarehe 14 Desemba 1973 lililotangaza Wilaya ya Mbulu na Hanang’. Chanzo kikubwa cha mgogoro huo ni baaadhi ya wananchi kutokukubaliana na alama za mipaka zilizopo kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Namba 266 la uanzishwaji wa Wilaya ya Mbulu na Wilaya ya Hanang’.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri za Wilaya ya Hanang na Mkalama zimetenga jumla ya shilingi milioni 40 kwa ajili ya kupima Vijiji vya Singa na Limbadau ambavyo ndio vipo kwenye eneo la mgogoro. Serikali inatarajia mgogoro huo utamalizika, ahsante sana.