Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kutatua mgogoro wa mipaka kati ya Jeshi la Magereza na wananchi wa Kata ya Ukondamayo hususan Kijiji cha Tumaini, Wilayani Urambo?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa heshima naomna niseme maneno machache kabla sijauliza maswali yangu ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, inasikitisha Serikali inapoacha migogoro inakua miaka na miaka na hili suala sio mara yangu ya kwanza kuuliza humu Bungeni, Mheshimiwa Masauni alipokuwa Naibu Waziri alijibu majibu ya hivyo hivyo. Kwa hiyo, naomba Wizara ikasome mafaili yake ya maswali itakuta ni hayo hayo majibu ni hayo na maswali ni hayo.

Maswali yangu ya nyongeza ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mgogoro huu umedumu tangu mwaka 1998 baada ya mipaka iliyokuwa halali kuondolewa na kupunguza maeneo ya wananchi ya kulima na kufuga mifugo yao, nini kauli ya Serikali kuhusu kumaliza mgogoro huu? Naomba Serikali itoe kauli yake lini inamaliza mgogoro uliodumu tangu mwaka 1998?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kama kweli Serikali ina nia ya kumaliza mgogoro huu ambao unawasikitisha sana wananchi wa Ukondamoyo na Tumaini, je, Waziri yupo tayari twende naye akaone yeye mwenyewe na ndiyo atakuja kuthibitisha kama kweli majibu yanayotolewa na Serikali ni ya halali? (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu na naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge yote mawili kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kama ulivyosema kwamba majibu ya msingi ya Serikali, mgogoro unaonekana haupo, ushahidi wa namna ambavyo Magereza walitoa lile eneo na kuligawanya kwa idadi ya heka ambapo Kijiji cha Tumaini kilipata heka 505, maelezo haya yanaonekana Mbunge hakubaliani nayo, ninaomba nikuhakikishie kwamba nipo tayari baada ya Bunge kwenda nikajionee mwenyewe na kuwasikiliza wananchi, ahsante sana. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kutatua mgogoro wa mipaka kati ya Jeshi la Magereza na wananchi wa Kata ya Ukondamayo hususan Kijiji cha Tumaini, Wilayani Urambo?

Supplementary Question 2

MHE. STANSALUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa Magereza nyingi zipo katikati ya mji kwa mfano Mji wa Maswa ipo katikati ya mji na majengo na maeneo yao yanaingiliana sana na makazi ya watu na maeneo hayo yanaonekana kuwa ni potential hata kwa uwekezaji mwingine.

Je, ni lini Serikali itaamua basi kujenga Magereza nje ya miji kwa mfano Maswa tumeshatoa na eneo na kuwapa Magereza ili wajenge nje ya mji na kuachia maeneo ya katikati ya mji kwa ajili ya uendelezwaji wa shughuli zingine za kibiashara? Ahsante sana. (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyongo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwa asili zamani huko kidogo maeneo haya yalikuwa pembeni ya miji, lakini kadri miji inavyokua tumejikuta sasa wakati mwingine maeneo haya ya Magereza na hata majeshi yakiwa katikati ya miji, jambo hili sio la kulijibu kwa haraka haraka kwa sababu ni mpango mkubwa unaohusisha Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Magereza au vyombo kama hivyo ambavyo vina changamoto kama hiyo.

Mheshimiwa Spika, wacha tulichukue tuone namna tunavyoweza kulifanya lakini si jambo jepesi kwa haraka kuhamisha gereza kwa mara moja na miundombinu yake, uwekezaji uliopo pale ni mkubwa lakini ni hoja ambayo kwa kweli Mheshimiwa Mbunge acha tuichukue tuitafakari.