Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 41 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 345 2021-06-01

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-

Je, Serikali inachukua hatua gani kutatua mgogoro wa mipaka kati ya Jeshi la Magereza na wananchi wa Kata ya Ukondamayo hususan Kijiji cha Tumaini, Wilayani Urambo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, napenda kukujulisha kwamba kwa sasa hakuna mgogoro wa ardhi kati ya Kata ya Ukondamoyo hususani Kijiji cha Tumaini na Gereza la Kilimo Urambo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli hapo awali ulikuwepo mgogoro baina ya vijiji vinne mojawapo Kijiji cha Tumaini. Mgogoro huo ulitatuliwa na kuhitimishwa mwaka 2000 kwa kushirikishwa viongozi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Ardhi, Jeshi la Magereza, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Urambo na Serikali ya vijiji vyote vinne vilivyokuwa na mgogoro kikiwemo Kijiji cha Tumaini.

Mheshimiwa Spika, hitimisho la mgogoro huo ni baada ya Jeshi la Magereza kukubali kutoa eneo la jumla ya ekari 3,218 kwa vijiji vilivyokuwa na mgogoro mojawapo Kijiji cha Tumaini kupewa ekari 505, Kijiji cha Imalamakoye ekari 195, Kijiji cha Nsendakanoge ekari 1,655 na Kijiji cha Itebulanda ekari 860.

Mheshimiwa Spika, aidha, hati ya makubaliano ya hitimisho la mgogoro ilisainiwa na viongozi wa vijiji vyote vinne vilivyokuwa na mgogoro kikiwemo Kijiji cha Tumaini na mawe ya mipaka (beacons) yakawekwa upya kwa utambulisho wa Namba Uv 66, Uv 69, Uv 107, Uv 35 na Uv 108, nakushukuru.