Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza:- Je Serikali ina mpango gani wa kutumia mashamba ya uzalishaji wa mbegu bora hususani za alizeti ambayo ndio zao la uti wa mgongo wa uchumi wa mkoa wa Singida?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri kuhusiana na upatikanaji wa mbegu ya alizeti kwa wananchi wa Mkoa wa Singida naomba nimuulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Mkoa wa Singida wamekuwa wakilima kwa utaratibu wa kawaida kabisa ule ambao wanalima wakimaliza wanaweka mbegu baada ya kuuza wanabakiza kidogo kwa ajili ya kwenda kulima tena mwakani ndio utaratibu wanaoutumia mpaka sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Naibu Waziri sasa yupo tayari kwa ajili ya kwenda kukutana na wakulima wa alizeti wa Mkoa wa Singida hususan jimbo la Singida Magharibi kwenye kata za Mwaru, Mgungia, Muhintiri, Minyukhe kwa ajili ya kwenda kuzungumza nao sasa kuona namna gani ambavyo ku-in cooperate mawazo yao na ya Wizara kwa ajili ya kuhakikisha kwamba upatikanaji wa mbegu ya alizeti, zinapatikana zenye tija ili walime kilimo ambacho sio cha desturi? Ahsante sana.(Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hanje kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwenda ku-visit tupo tayari na tutafanya hivyo na Mwenyezi Mungu akijaalia mwezi huu wa Juni tutakuwa na Mkutano mkubwa utakaoongozwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu katika Mkoa wa Sindiga kwa ajili ya suala la zao la alizeti na kukutana na wazalishaji na wakulima wa alizeti. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza:- Je Serikali ina mpango gani wa kutumia mashamba ya uzalishaji wa mbegu bora hususani za alizeti ambayo ndio zao la uti wa mgongo wa uchumi wa mkoa wa Singida?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, naomba commitment ya Serikali au itusaidie Serikali kuona namna iliyobora hasa kwa mbegu ambayo inaitwa Hysun inauzwa shilingi 35,000 kwa kilo mbili.

Je, Serikali sasa ipo tayari kuingiza ruzuku kwa mbegu hii ili uzalishaji wa mafuta uwe bora zaidi katika Mkoa wa Singida na mikoa mingine ambayo inalima alizeti?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri kwamba gharama ya mbegu za highbred za alizeti ni kubwa sana na sio rahisi mkulima wa kawaida kuweza kuzinunua. Kwa hiyo, mpango wa Wizara ya Kilimo kwa mwaka ujao wa fedha baada ya kupitishiwa bajeti yetu hapa ni kwamba tukimaliza mkutano wa kukutana Singida na wazalishaji wote wa viwanda vya kulizisha mafuta mpango wetu ni kutengeneza subsidy, ruzuku ili bei ya mbegu hizo kwa utaratibu tutakaoweka kwa wasambazaji ili wakulima bei yao iweze kupungua.

Kwa hiyo huo ni sehemu mpango wetu na tunaamini tutautumia katika mwaka ujao wa fedha ili kuweza kupunguza bei ya mbegu za alizeti.