Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 40 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 336 2021-05-31

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza:-

Je Serikali ina mpango gani wa kutumia mashamba ya uzalishaji wa mbegu bora hususani za alizeti ambayo ndio zao la uti wa mgongo wa uchumi wa mkoa wa Singida?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mchango wa zao la alizeti katika kuongeza upatikanaji wa mafuta ya kula hapa nchini ambapo asilimia 68 ya mafuta ya kula yanatokana na zao hilo ikilinganishwa na mazao mengine ya yanayochangia asilimia 31.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuweka mikakati ya kuongeza upatikanaji wa mbegu bora za mafuta nchini kwa kutenga fedha jumla ya shilingi bilioni 40 katika mwaka wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji kwenye mashamba ya uzalishaji wa mbegu ya Wakala wa Mbegu wa Serikali ili kuzalishaji mbegu za alizeti na mazao mengine.

Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu hiyo kutawezesha kuongeza uzalishaji wa mbegu za alizeti kutoka tani 538 katika msimu wa 2019/2020 hadi kufikia tani 10,000 za mbegu bora za alizeti mwaka wa fedha 2019/2030 ambazo zitatosha kutumika katika eneo la hekta milioni 1.2 zinazoweza kuzalisha tani 500,000 za mafuta ya kula.

Mheshimiwa Spika, kwa kuthamini umuhimu wa zao la alizeti, Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi imeendelea kugundua na kuzalisha aina mpya ya mbegu bora za alizeti zenye sifa ya kutoa mavuno na mafuta mengi na zenye ukinzani dhidi ya magonjwa kutoka aina 1 hadi 17 za zao la alizeti katika msimu wa 2019/2020.