Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka na kuongeza vifaa tiba na wataalam katika vituo vya afya ilivyojenga vikiwemo vifaa tiba maalum kama vile “incubator beds” na taa maalum kwa ajili ya kukabiliana na homa ya manjano kwa watoto njiti?

Supplementary Question 1

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa tayari kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa vifaa tiba lakini pia bado kuna tatizo la ukosefu wa vyumba vya kuhudumia hawa watoto njiti katika vituo vyetu vya afya pamoja na Hospitali zetu za Wilaya.

Je, Serikali inamkakati gani katika kuhakikisha kila Hospitali yetu ya Wilaya navituo vya afya inakuwa na vyumba hivyo kwa ajili ya kuhudumia watoto hao?

Mheshimiwa Spika, swali lapili pale Mererani tuna kituo kikubwa cha afya ambacho kinahudumia kata zaidi ya nne katika Wilaya ya Simajanjiro na Wilaya za jirani kama Hai na Arusha DC, lakini tatizo kubwa lililopo pale hawana kabisa chumba maalum cha kuhifadhia maiti, hivyo ndugu zetu wanapotangulia mbele za haki ndugu wanahangaika kuwasafirisha kwenda Mount Meru na Himo.

Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kukamilisha jengo lililojengwa tayari ili huduma hiyo iweze kupatikana pale katika Kituo cha Afya cha Mererani? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika ujenzi wa majengo ya huduma ya afya ya uzazi na mtoto ambayo yanaendelea nchini kote hivi sasa ramani zile zimezingatia provision ya kuwa na chumba kwa ajili ya watoto wanaozaliwa kabla ya muda wao maarufu kama njiti. Kwa hiyo ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika michoro ya sasa ramani zetu zimezingatia kuwa na vyumba ambavyo vitakuwa mahsusi na vitawekewa vifaa tiba zikiwemo Radiant Warmers kwa ajili ya kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya muda wao.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo Serikali imeendelea pia kuhakikisha inaelimisha jamii kuhusiana na kangaroo mother care kwa maana ya huduma mwambata pamoja na kuwa vyumba hivyo. Kwa hiyo tutaendelea kuhakikisha kwamba vyumba hivyo vinakamilishwa.

Mheshimiwa Spika, lakini pili chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha afya cha Mererani ni muhimu sana na mimi ninaomba tulichukue hili tutawasiliana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa maana ya Simanjiro lakini na sisi kama Serikali kuu tutaona njia bora zaidi ya kuhakikisha tunatafuta fedha kwa ajili ya kujenga chumba cha kuhifadhia maiti. Ninakushukuru sana. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka na kuongeza vifaa tiba na wataalam katika vituo vya afya ilivyojenga vikiwemo vifaa tiba maalum kama vile “incubator beds” na taa maalum kwa ajili ya kukabiliana na homa ya manjano kwa watoto njiti?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana, Kituo cha Afya cha Kidatu Nyandeo kina uhaba mkubwa sana wa jokofu la kuhifadhia miili ya marehemu na mara ya mwisho tuliwasiliana na MSD wakasema kwamba wangepeleka jokofu hilo lakini mpaka sasa hawajapeleka.

Je, lini Serikali itapeleka Jokofu katika Kituo cha Afya cha Nyandeo Tarafa ya Kidatu Jimbo la Kilombero?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abubakari Asenga, Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuweka mipango ya kupata vifaa tiba na vifaa mbalimbali yakiwemo majokofu ya kuhifadhia maiti, lakini pamoja na jitihada za Serikali tumeendelea pia kuhakikisha tunawaelekeza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali kuona umuhimu wa kutenga fedha katika mapato ya ndani kununua baadhi ya vifaa tiba na baadhi ya vitendea kazi katika hospitali zetu yakiwemo majokofu ya kuhifadhia maiti.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninaomba nichukue nafasi hii kumwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero kwa sababu majokofu haya ni kati ya Milioni 12 hadi Milioni 30; fedha hii ipo ndani ya uwezo wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilombero na hivyo ninamuelekeza katika mwaka ujao wa fedha wahakikishe wanaweka provision ya kununua jokofu la kuhifadhia maiti katika kituo cha afya. Nakushukuru sana.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka na kuongeza vifaa tiba na wataalam katika vituo vya afya ilivyojenga vikiwemo vifaa tiba maalum kama vile “incubator beds” na taa maalum kwa ajili ya kukabiliana na homa ya manjano kwa watoto njiti?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa tayari kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa vifaa tiba lakini pia bado kuna tatizo la ukosefu wa vyumba vya kuhudumia hawa watoto njiti katika vituo vyetu vya afya pamoja na Hospitali zetu za Wilaya.

Je, Serikali inamkakati gani katika kuhakikisha kila Hospitali yetu ya Wilaya navituo vya afya inakuwa na vyumba hivyo kwa ajili ya kuhudumia watoto hao?

Mheshimiwa Spika, swali lapili pale Mererani tuna kituo kikubwa cha afya ambacho kinahudumia kata zaidi ya nne katika Wilaya ya Simajanjiro na Wilaya za jirani kama Hai na Arusha DC, lakini tatizo kubwa lililopo pale hawana kabisa chumba maalum cha kuhifadhia maiti, hivyo ndugu zetu wanapotangulia mbele za haki ndugu wanahangaika kuwasafirisha kwenda Mount Meru na Himo.

Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kukamilisha jengo lililojengwa tayari ili huduma hiyo iweze kupatikana pale katika Kituo cha Afya cha Mererani? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika ujenzi wa majengo ya huduma ya afya ya uzazi na mtoto ambayo yanaendelea nchini kote hivi sasa ramani zile zimezingatia provision ya kuwa na chumba kwa ajili ya watoto wanaozaliwa kabla ya muda wao maarufu kama njiti. Kwa hiyo ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika michoro ya sasa ramani zetu zimezingatia kuwa na vyumba ambavyo vitakuwa mahsusi na vitawekewa vifaa tiba zikiwemo Radiant Warmers kwa ajili ya kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya muda wao.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo Serikali imeendelea pia kuhakikisha inaelimisha jamii kuhusiana na kangaroo mother care kwa maana ya huduma mwambata pamoja na kuwa vyumba hivyo. Kwa hiyo tutaendelea kuhakikisha kwamba vyumba hivyo vinakamilishwa.

Mheshimiwa Spika, lakini pili chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha afya cha Mererani ni muhimu sana na mimi ninaomba tulichukue hili tutawasiliana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa maana ya Simanjiro lakini na sisi kama Serikali kuu tutaona njia bora zaidi ya kuhakikisha tunatafuta fedha kwa ajili ya kujenga chumba cha kuhifadhia maiti. Ninakushukuru sana. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka na kuongeza vifaa tiba na wataalam katika vituo vya afya ilivyojenga vikiwemo vifaa tiba maalum kama vile “incubator beds” na taa maalum kwa ajili ya kukabiliana na homa ya manjano kwa watoto njiti?

Supplementary Question 4

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana, Kituo cha Afya cha Kidatu Nyandeo kina uhaba mkubwa sana wa jokofu la kuhifadhia miili ya marehemu na mara ya mwisho tuliwasiliana na MSD wakasema kwamba wangepeleka jokofu hilo lakini mpaka sasa hawajapeleka.

Je, lini Serikali itapeleka Jokofu katika Kituo cha Afya cha Nyandeo Tarafa ya Kidatu Jimbo la Kilombero?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abubakari Asenga, Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuweka mipango ya kupata vifaa tiba na vifaa mbalimbali yakiwemo majokofu ya kuhifadhia maiti, lakini pamoja na jitihada za Serikali tumeendelea pia kuhakikisha tunawaelekeza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali kuona umuhimu wa kutenga fedha katika mapato ya ndani kununua baadhi ya vifaa tiba na baadhi ya vitendea kazi katika hospitali zetu yakiwemo majokofu ya kuhifadhia maiti.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninaomba nichukue nafasi hii kumwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero kwa sababu majokofu haya ni kati ya Milioni 12 hadi Milioni 30; fedha hii ipo ndani ya uwezo wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilombero na hivyo ninamuelekeza katika mwaka ujao wa fedha wahakikishe wanaweka provision ya kununua jokofu la kuhifadhia maiti katika kituo cha afya. Nakushukuru sana.