Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kusamehe kodi za miaka ya nyuma Taasisi za Dini zilizokuwa zikiendeshwa kwa utaratibu usiolenga kupata faida na kuziwekea utaratibu Taasisi hizo kuanza kulipa tangu walipojulishwa kutakiwa kulipa kodi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwanza naipongeza Serikali kwa majibu hayo na hasahasa kupima viwanja 56,792 katika kipindi kidogo cha miezi tisa, lakini Sikonge pale Mjini niao wananchi 2000 kwenye maeneo ya Ukanga wana viwanja 1400 na Majengo viwanja 6000 jumla viwanja 2000 kwa muda mrefu sana zaidi ya miaka 10 wanaomba hati hawajapatiwa.

Mheshimiwa Spika, sasa je, swali langu la kwanza wizara inawasaidieje wananchi wa Sikonge waweze kupata hati zao kwa haraka?

Mheshimiwa Spika, la pili je, Serikali haioni kwamba sasa hivi hapa nchini kuna uchumi mgumu kiasi ambacho wananchi wanapata shida kupata laki 150 kwenye miji ya vijiji kama Sikonge kupima kiwanja kimoja je, Serikali haioni kwamba hasa kuna wakati umefika wa kuwapa ruzuku ili waweze kupata hati zao za ardhi.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kakunda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza anataka kujua tu kwamba ni lini utoaji hati utafanyika katika maeneo hayo. Tayari tulishafungua ofisi za mikoa na katika kasi ya utoaji hati sasa hivi inakwenda kwa kasi kubwa naomba nimuhakikishie tu kwamba ofisi yetu ya Tabora Mjini itakwenda kukamilisha hiyo na kwa kupitia majibu ninayotoa sasa basi wafike katika hayo maeneo mawili ndani ya Sikonge yenye viwanja 2000 ambao nasema kwamba hawajapewa hati mpaka leo, iwapo watakuwa wamekamilisha taratibu zote za umilikishaji.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anazungumzia suala la ruzuku kwamba 150,000 katika suala zima la upimaji ni gharama kubwa. Naomba niseme tu kwamba gharama hii si kubwa kama tunavyofikiri lakini pia inategemea na eneo husika maana kuna maeneo mengine mpaka sasa wanalipa 60,000 wanalipa 90,000. Wakiwa watoaji ni wachache unakuta kwamba ile gharama hata ya yule anayeenda kupima inakuwa kidogo ni kubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kuwa na watu wengi kwa wakati mmoja wanayohitaji gharama zile zinashuka kwa hiyo gharama zinashuka kutegemeana na volume ya kazi ambayo mpimaji anakwenda kufanya pale. Niwaombe wananchi kwamba suala la urasimishaji linakwenda kuisha 2023 kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kwa sababu ilikuwa programu ya miaka kumi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, waongeze kasi sasa hivi ili kazi ile iishe halafu tuendelee na upimaji wa kawaida ambao hautakuwa na zoezi la urasilimishaji ambao majengo yale yamekaa kiholela na upimaji wake unakuwa kidogo ni mgumu ahsante.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kusamehe kodi za miaka ya nyuma Taasisi za Dini zilizokuwa zikiendeshwa kwa utaratibu usiolenga kupata faida na kuziwekea utaratibu Taasisi hizo kuanza kulipa tangu walipojulishwa kutakiwa kulipa kodi?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika nashukuru, changamoto ambayo inakumba Sikonge ya ujenzi holela inakumba pia jiji la Dar es Salaam sasa tofauti na Sikonge Dar es Salaam tayari tuna Dar es Salaam City Master Plan ya 2012 mpaka 2032 ambayo tumeshaipitisha katika ngazi zote inasubiri tu utekelezaji. S nataka waziri uniambaie ni lini Serikali itaanza kutekeleza mkakati wa Dar es Salaam City Master Plan ili mji wetu upangike vizuri na uonekane na changamoto zote za mji kutokupangwa?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Halima Mdee Mbunge wa viti maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Dar es salaam tayari inayo master plan na ilishapitia katika nganzi zote lakini changamoto iliyopo pale katika utekelezaji wake bado katika halmashauri zinazohusika katika kufanya kazi ile kwa sababu ule utekelezaji unakwenda awamu kwa awamu kutegemeana na utaratibu wa mpangilio wa majenzi waliyoyaweka.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa sasa utekelezaji unaoendelea hawaruhusu pia hata katika ujenzi unaoendelea kuweza kujenga nyumba pengine katika maeneo ambayo master plan inazungumzia habari ya kwamba pana magorofa kadhaa, ukiomba kujenga nyumba ya kawaida unazuiliwa. Kama ni eneo la viwanda ukiomba kujenga nyumba ya kawaida unazuiliwa. Kwa hiyo, utekelezaji umeanza japokuwa space yake ni ndogo kutegemea jinsi mtu mji wenyewe wa Dar es Salaam ulivyokuwa umejengeka katika taratibu ambazo si ki mipango miji katika maeneo mengi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, lazima twende nao taratibu namna ya kuweza adapt kile ambacho tayari kimepangwa na wenye halmashauri zao ili kuweza kuhakikisha ile master plan inatekelezwa. Kwa hiyo, sisi kama wizara tutaendelea kushirikiana na TAMISEMI ili kuweza kuona ni jinsi gani ile master plan inatekelezwa bila kuleta athari kwa wananchi.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kusamehe kodi za miaka ya nyuma Taasisi za Dini zilizokuwa zikiendeshwa kwa utaratibu usiolenga kupata faida na kuziwekea utaratibu Taasisi hizo kuanza kulipa tangu walipojulishwa kutakiwa kulipa kodi?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza, Halmashauri ya Geita Vijijini yenye makao makuu yake Nzela tumepima viwanja vikakamilika mwezi wa 12 mwaka jana na mwezi wa kwanza tulileta barua ya maombi kwa ajili ya kupitisha ile kamati ya ugawaji wa viwanja toka mwezi wa kwanza mpaka leo hatujawahi kupata majibu kutoka Ofisi ya Katibu Mkuu ambaye ndio mwenye idhini ya kuidhinisha hiyo kamati.

Je nini kauli ya Serikali kuhusiana na barua hiyo ya kuidhinisha hiyo kamati ilituendelee kuuza viwanja ambavyo viko tayari?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba nilichukuwe swali la Mheshimiwa Musukuma kama alivyosema kama kweli wameshaleta ofisini nikitoka hapa mchana nakwenda kuangalia kama yapo na tuweze kujua kwa nini mpaka leo haijaidhinishwa. Kwa sababu taratibu tunasema kamati zile zikishaletwa kazi ya waziri ni kuweza kuridhia ili zikaanze kufanya kazi. Sasa haiwezekana iwe imekuja kwa muda wote huo halafu majibu hajapa naomba nilichukuwe ili mchana niweze kuangalia nitampa majibu yake.