Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa Mikopo ya Elimu ya Juu kwa Watu wenye Ulemavu kama ruzuku badala ya mikopo kama ilivyo sasa?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa kuweka ulemavu kama kigezo kimojawapo cha upatikanaji wa mikopo kama ambavyo Bunge la Kumi na Moja liliweza kushauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali hili si mara yangu ya kwanza naliuliza ndani ya Bunge hili, lakini pia mara kadhaa nilipopata kuchangia niliweza kuchangia na jibu limekuwa ni hili. Kama ambavyo jibu limesema kwamba Serikali italifanyia kazi, ni lini Serikali itaanza kulifanyia kazi? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SANYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ikupa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishajibu katika majibu yangu ya swali la msingi kwamba Serikali inaendelea kulifanyia kazi suala hili. Kama nilivyokwishaeleza hapa punde kwamba katika mjadala wetu wa bajeti tulisema kwamba tunakwenda kuwa na mjadala mpana kuhusiana na elimu yetu nchini kwa maana kwamba tunaenda kuangalia Sera yetu ya Elimu ya mwaka 2014, lakini tunaenda kuangalia Sheria yetu ya Elimu ya mwaka 1978. Hili nalo kwenye mjadala huo litakwenda kujadiliwa kwa kina na kuona ni namna gani tunaweza kuyafikia makundi haya badala ya kuwapa mikopo tukatoa ruzuku. Nadhani kabisa katika mjadala huo tunaweza tukayaingiza.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.