Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 36 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 299 2021-05-25

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa Mikopo ya Elimu ya Juu kwa Watu wenye Ulemavu kama ruzuku badala ya mikopo kama ilivyo sasa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo (SURA 178) ambayo inabainisha kuwa fedha na mikopo hiyo ni kwa ajili ya wanafunzi wahitaji (needy) wenye sifa za kujiunga na taasisi za elimu ya juu (eligible). Lengo la matakwa haya ya kisheria ni kuwawezesha wanafunzi wote wahitaji, wenye ulemavu na wasio na ulemavu, wanaotoka kwenye familia zenye uwezo mdogo wa kiuchumi kufikia ndoto zao za kupata elimu ya juu.

Mheshimiwa Spika, sheria pia inaipa Bodi mamlaka ya kuweka vigezo vya ziada ambapo katika mwaka wa masomo 2020/2021, Mwongozo wa Utoaji Mikopo ulitoa kipaumbele kwa makundi maalum wakiwemo wenye ulemavu au waombaji mkopo wenye wazazi wenye ulemavu. Kwa kutumia kigezo hiki, katika mwaka wa masomo 2020/ 2021, jumla ya wanafunzi 92 wenye ulemavu au wazazi wenye ulemavu walipangiwa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 350.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kutoa ruzuku badala ya mikopo, Serikali italifanyia kazi kwa kuzingatia dhana nzima ya utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wenye uhitaji na kuwa na mfuko endelevu wa mikopo ya elimu ya juu nchini.