Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Jengo la Utawala la Central Police Njombe?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Spika, asante. Kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Njombe, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; Serikali imesema kwamba, wanatafuta hizi fedha shilingi milioni 322. Ningependa kujua mkakati mzima wa upatikanaji wa hizi fedha na zitakuwepo kwenye bajeti ipi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; eneo ambalo wamepanga kujenga Ofisi ya Mkoa wa Njombe (Central Police), ni eneo hilohilo Ofisi ya Mkoa imepangwa kujengwa na Mahakama ya Mkoa; Ofisi ya Mkoa na Mahakama zimeshajengwa, sasa hii bado.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Njombe wangependa kujua ni lini hasa ofisi hii itajengwa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Njombe, maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza Mheshimiwa anauliza; je, katika bajeti hii tumepanga kuweza kupata hizo fedha?

Mheshimiwa Spika, kubwa tu nimwambie kwamba katika bajeti hii hakuna fungu hili, lakini tutajitahidi katika bajeti ijayo pesa hizi ziwepo na tumuahidi Mheshimiwa kwamba, tutampa kipaumbele katika kuhakikisha kwamba, eneo hili linapata kituo hicho cha polisi ambacho kitatoa huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, lakini je, ni lini sasa Serikali italipa hiyo fidia? Nimwambie tu kwamba, tutajitahidi na tumuahidi mwaka ujao wa fedha tutajitahidi tulipe hiyo fidia, ili sasa ujenzi huu uweze kuanza haraka na wananchi waweze kupata huduma hizo za ulinzi na usalama. Nakushukuru.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Jengo la Utawala la Central Police Njombe?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante na nashukuru kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni je, Serikali inatumia utaratibu gani wa kulipa madeni ya askari ambao unaendelea kwa kuwa wameanza kulipa 2018/2019 na wameacha 2017, lakini pia askari waliopandishwa vyeo kutoka Mainspekta kuwa Warakibu wa Polisi 99, askari 99 ambao walipanda mwaka 2013 mpaka 2017 hawajalipwa mshahara kwa cheo hicho wameanza kulipwa 2018? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali hili la Mheshimiwa Jesca kwamba suala hili ni suala ambalo linahitaji takwimu na linahitaji data za uhakika. Kwa hiyo, kubwa tu nimwambie Mheshimiwa kwamba pamoja na kwamba utaratibu umeshaanza kupangwa, lakini nimuombe tu kwamba, suala hili aendelee kulipa muda ili tukalifanyie kazi halafu tutajua namna ya kuja kumjibu, nakushukuru.