Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 39 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 330 2021-05-28

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Jengo la Utawala la Central Police Njombe?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pindi Hazara Chana, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Njombe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, jengo la ofisi zinazotumika kwa sasa kama jengo la polisi la utawala (Central Police) Mkoa wa Njombe lipo katika hifadhi ya barabara kuu iendayo Mkoa wa Ruvuma. Kwa sasa Jeshi la Polisi limeshaomba eneo toka Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa ajili ya kujenga ofisi za utawala na makazi ya askari na Halmashauri imeshatoa hekari 40 eneo la Lunyunyu.

Mheshimiwa Spika, tathmini kwa ajili ya kulipa fidia wananchi walioko eneo hilo imeshafanyika kupitia Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe na kiasi cha shilingi 322,000,000 zinahitajika kwa ajili ya malipo ya fidia na kwa sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kulipa fidia hii ili ujenzi uanze mara moja. Nakushukuru.