Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara tatu za Lukoma – Lubalisi, Kalya – Ubanda na Kalya – Sibwesa zinazounganisha Mkoa wa Kigoma kupitia Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, naomba niishukuru Serikali kwa majibu mazuri yaliyotolewa mbele hapa, lakini ninalo swali moja la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jimbo langu la Kigoma Kusini linao urefu wa barabara hii ya Simbo kwenda Kalya ndio hiyo ambayo inazalisha hizo barabara tatu nilizozisema. Barabara ya Kalya kwenda Sibwesa inatoka nje ya nchi kwa sababu kuna bandari pale Sibwesa, lakini barabara hii pia ya Lubalisi inatoka nje ya mkoa na hii ya Kalya – Ubanda inatoka nje ya mkoa.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naiomba Serikali iangalie kuweza kuipa kipaumbele barabara hizi kwa sababu zinaufungua mkoa kupitia Halmashauri ya Kigoma Kusini kwa maana ya Jimbo la Kigoma Kusini, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge alichoomba ni kwamba Serikali tuizingatie ile barabara na mimi nipokee ombi lake kwa sababu tumeshakiri katika jibu letu la msingi kwamba moja hiyo barabara tumeitambua na kuiingiza katika mpango. Awali TARURA wakati inaanzishwa tulikuwa tulikabidhiwa barabara zenye urefu wa kilometa 108,000; kwa hiyo sasa hivi kuna ongezeko la barabara karibu 36,000 mpya.

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa barabara hizo ambazo zimetambulika ni pamoja na hizi barabara ambazo Mheshimiwa Mbunge umeziainisha. Kwa hiyo, kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha na tutakavyoendelea kuziweka katika mpango basi barabara hiyo tutaipa kipaumbele katika mwaka wa fedha unaokuja.