Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 322 2021-05-28

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara tatu za Lukoma – Lubalisi, Kalya – Ubanda na Kalya – Sibwesa zinazounganisha Mkoa wa Kigoma kupitia Wilaya ya Uvinza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, asante sana; kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020 barabara za Lukoma - Lubalisi, Kalya - Ubanda na Kalya - Sibwesa zilitambuliwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) na kuwekwa kwenye mfumo wa barabara zinazotambuliwa na TARURA (DROMAS). Barabara hizo zitaingizwa kwenye mpango wa matengenezo ya barabara kupitia fedha za matengenezo ya barabara zinazotolewa kwa TARURA katika kila Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Wananchi pamoja na Shirika la Maendeleo la Ubelgiji la Kuendeleza Kilimo – Kigoma (SAKIRP) inaendelea na ujenzi wa madaraja 10 kwa kutumia teknolojia ya mawe kwa gharama ya shilingi milioni 190 ambapo madaraja matatu yamekamilika likiwemo Daraja la Mto Ruega katika barabara ya Kalya – Ubanda lililojengwa kwa shilingi milioni 37 katika mwaka wa fedha 2019/2020.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha katika bajeti zake ili kuzifanyia matengenezo barabara hizo kwa kadiri upatikanaji wa fedha utakavyoendelea kuimarika.