Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:- Je, ni nini mpango wa Serikali kuwawezesha akina baba kiuchumi baada ya mpango wa Halmashauri wa kuwawezesha akina mama, vijana na watu wenye ulemavu kuwa na mafanikio makubwa?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Wizara; na kwa kuwa katika kundi la vijana wanakopeshwa vijana wa kiume na wa kike; na kutokana na Katiba yetu tunawatambua kwa umri wa miaka 18 mpaka 35; na kwa kuwa kuna wanaume wengi ambao ndiyo bread winner kwenye familia zao na ni wazalishaji kati ya miaka 36 – 45; na kwa sababu ni suala la kisera: Je, Serikali ipo tayari kuongeza umri angalau mpaka miaka 45 katika kundi hili la vijana ili wanaume waweze kufaidika na mikopo hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA – (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, Serikali imeweka utaratibu huu wa mikopo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Na katika kundi la vijana asilimia kubwa wanaonufaika na mikopo hii ni vijana wa kiume, lakini definition kwa maana ya tafsiri ya vijana kwa mujibu wa taratibu zetu ni wale wenye umri wa miaka 18 hadi 35. Kwa hivyo, kwa maana ya tafsiri hii ya kisheria Serikali bado haijaweka mpango wa kuongeza umri kwa sababu, lengo la mikopo hii ni kwa vijana na kwa maana ya tafsiri ya vijana ni chini ya miaka 35. Kwa hivyo tunachukua wazo lake, lakini kwa sasa sheria hii itaendelea kutekelezwa wakati tunafanya tathmini ya kuona uwezekano wa kuongeza eneo hilo.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:- Je, ni nini mpango wa Serikali kuwawezesha akina baba kiuchumi baada ya mpango wa Halmashauri wa kuwawezesha akina mama, vijana na watu wenye ulemavu kuwa na mafanikio makubwa?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni kweli kwamba, katika halmashauri zetu kunatengwa fedha asilimia 10 kwa maana ya mbili, nne na nne kwa wanawake, lakini ufuatiliaji wa mkopo huu baada ya kupewa hivyo vikundi unakuwa ni mgumu sana kurudisha fedha kwenye halmashauri. Serikali ina mkakati gani wa kudai madeni hayo ili fedha zirudi zikopeshe wanawake wengine kwa wakati unaofuata? Ahsante.

SPIKA: Mheshimiwa, swali linahusu wanaume nao watapataje access ya hizo fedha?

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, wanaume tunaomba wapate, lakini wanapokwenda kukopa huwa hawaelezi wake zao kama wamekwishakopa mkopo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA – (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mpango huu wa kukopesha asilimia kumi kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu Serikali imeboresha utaratibu kupitia Sheria Na. 12 ya Mikopo kwa maana ya fedha za Mamlaka ya Serikali za Mitaa, kuhakikisha sasa siku za nyuma hatukuwa na asilimia kwa ajili ya ufuatiliaji wa marejesho ya mikopo hii. Kwa hivyo, ilikuwa ni ngumu kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii kufuatilia vikundi ambavyo vimekopeshwa kwa ajili ya kurejesha mikopo ile ili vikundi vingine vinufaike zaidi.

Mheshimiwa Spika, lakini kuanzia mwaka wa fedha ujao tumeweka kifungu cha ufuatiliaji katika vikundi hivyo kuwawezesha Mamlaka ya Serikali za Mitaa na Maafisa Maendeleo ya Jamii kufuatilia vikundi vile pamoja na kuviwezesha kuhakikisha marejesho yanafanyika ipasavyo.