Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 316 2021-05-27

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:-

Je, ni nini mpango wa Serikali kuwawezesha akina baba kiuchumi baada ya mpango wa Halmashauri wa kuwawezesha akina mama, vijana na watu wenye ulemavu kuwa na mafanikio makubwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimeendelea kuwezesha wananchi kiuchumi kwa kutoa mikopo isiyo na riba kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Mikopo hiyo hutolewa kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290 kifungu cha 37A inayoelekeza kutenga 10% ya mapato yanayokusanywa na Halmashauri kwa ajili ya mikopo ya 4% kwa wanawake, 4% kwa vijana na 2% kwa watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Spika, lengo la mikopo hii ni kusaidia makundi maalum katika jamii ambayo hayawezi kupata mikopo katika mabenki ya biashara na taasisi za fedha kwa sababu ya masharti magumu ikiwemo dhamana na riba kubwa. Hivyo, Serikali ilitoa kipaumbele kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa kuwa wengi wao hawakopesheki katika mabenki na taasisi za fedha. Kwa sasa Serikali haikusudii kuanzisha mpango wa kuwawezesha wanaume au akina baba katika mikopo hii.