Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza upatikanaji wa maji katika Mji wa Ruanda Wilayani Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini nina swali moja dogo la nyongeza. Mradi wa Maji wa Litembo una uchakavu mkubwa wa miundombinu hali iliyopelekea Kijiji cha Langandondo kukosa maji kwa miaka minne mvululizo, lini mradi huu unaenda kukarabitiwa na wananchi wale wa Langandondo waweze kupata maji Kata ya Litembo. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Liuka Benaya, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, uchakavu wa Mradi wa Litembo kama Wizara tunautambua na tayari tumetoa maagizo kwa Meneja wa RUWASA tayari na yeye anaendelea kujipanga ili kuhakikisha kwamba mwaka ujao wa fedha nao tuweze kutupia jicho la utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumpongeza Mheshimiwa Liuka amekuwa ni mfuatiliaji mzuri, tumeondoka hapa wakati wa weekend tumekwenda Mbinga Vijijini tumefanya kazi nzuri na miradi hii yote ya uchakavu pale anafahamu tulishakubaliana utekelezaji wake utafanyika kwa haraka.