Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 37 Water and Irrigation Wizara ya Maji 312 2021-05-26

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza upatikanaji wa maji katika Mji wa Ruanda Wilayani Mbinga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Liuka Kapinga Benaya, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Ruanda unakua kwa kasi hivyo kuongezeka kwa mahitaji ya maji kufikia wastani wa ujazo wa lita 210,100 kwa siku ikilinganishwa na uzalishaji wa sasa wa ujazo wa lita 162,000 kwa siku. Serikali katika mwaka 2021/2022 imepanga kukarabati Mradi wa Maji Ruanda ambapo kazi zitakazofanyika ni pamoja na kujenga vituo 15 vya kuchotea maji, kujenga chemba moja ya kugawa kwenda kwenye njia kuu, kufanya ukarabati wa chanzo, kulaza bomba njia kuu na njia ya usambazaji umbali wa kilometa 22.9 pamoja na ukarabati wa matanki mawili ya kuhifadhia maji ya ujazo wa lita 50,000 na 75,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 1.39 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maji Wilayani Mbinga ukiwemo ukarabati wa Mradi wa Ruanda kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa maji katika Mji wa Ruanda.