Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini wananchi wa Kata ya Ugalla watapatiwa umeme wa REA III?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Hii Kata ya Ugalla na huo mradi anaosema umeanza mwezi Machi, lakini hakuna dalili yoyote ya mradi, hakuna kitu chochote; na wananchi katika kata hiyo wamesubiri kwa muda mrefu, ni kata; kuna Kata ya Litapunga na Ugala wana miaka mingi wanaona wenzao wanapata umeme lakini wenyewe hawajawahi kupata umeme wala dalili ya nguzo hamna, lakini hapa ameniambia kuwa mwezi Machi mradi umeanza. Sasa hapo kidogo napata wasiwasi kwa sababu hamna dalili kabisa, hakuna dalili ya umeme. Sasa naomba basi Naibu Waziri aji-commit twende akaone ili ajue hali halisi ya wananchi kwa jinsi wanavyopata tabu.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; wananchi katika vijiji vingine wanalipia umeme Sh.27,000, lakini wanachukua muda mrefu sana miezi sita, saba mpaka nane hawaingiziwi umeme, basi Waziri atueleze wakilipa inachukua muda gani ili wananchi wanaweza kupata umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Lupembe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi wa upelekaji umeme wa awamu ya tatu, mzunguko wa pili, ulisainiwa na kuzinduliwa rasmi mwezi Machi na hatua kwa hatua zimekuwa zikianza sehemu moja moja kuendelea. Kwa mfano Mtwara wameendelea, Jumamosi iliyopita Mheshimiwa Waziri alizindua tena Arusha, kwa hiyo kufikia Disemba mwakani ndio maeneo yote yatakuwa yamekamilika. Kuna maeneo mengine yameshaanza, mengine bado yanaendelea, lakini hatua za kupeleka nguzo zimeanza. Kwa hiyo uzinduzi ndio ulikuwa mwezi Machi mwaka huu.

Mheshimiwa Spika, kwenye maeneo mengine kama alivyosema kwake, watu wanapolipa umeme zinachukuliwa zile hatua sasa za kupeleka vifaa mbalimbali kwa wale wananchi waliolipia kama nguzo kama waya kwa pamoja ili sasa tuweze kufunga kwa pamoja. Hata hivyo, tunachofanya tunaweka utaratibu angalau tuseme ndani ya mwezi mmoja, kila mtu aliyelipia umeme awe ameupata kulingana na mazingira aliyokuwa nayo. Pengine kwenye three phase inachukua hadi pengine siku 90, lakini tumekuwa tukijitahidi kuhakikisha kwamba kila aliyelipia umeme anaupata na anaupata kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jibu lake la msingi.

Mheshimiwa Spika, ni kweli utelekezaji wa mradi kambambe wa awamu ya tatu, round ya pili umeanza rasmi toka mwezi Machi mwaka huu na wakandarasi wote wameshakwenda site. Kesho tuna mkutano wa wakandarasi wote hapa Dodoma, kuwaarifu watoe taarifa kwa Waheshimiwa Wabunge na Madiwani katika maeneo yao. Kwa hiyo inawezekana Mheshimiwa Mbunge kweli hajakutana nao, lakini wameshaanza kazi rasmi na wanakwenda kila eneo kwenye maeneo ambako wamepangiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, nitoe taarifa tu kwa wakandarasi kupitia Bunge lako Tukufu kwamba, wakandarasi wote wakaripoti kwa Waheshimiwa Wabunge wanapoingia katika maeneo yao ili Waheshimiwa Wabunge wapate taarifa hizo. (Makofi)

Name

Job Yustino Ndugai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kongwa

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini wananchi wa Kata ya Ugalla watapatiwa umeme wa REA III?

Supplementary Question 2

Je, ni lini wananchi wa Kata ya Ugalla watapatiwa umeme wa REA III?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kata ya Ugalla pamoja na vijiji tisa, wataanza kupatiwa umeme kuanzia mwezi Juni mwaka huu mpaka mwezi Mei mwaka ujao. (Makofi)