Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 35 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 291 2021-05-24

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, ni lini wananchi wa Kata ya Ugalla watapatiwa umeme wa REA III?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na utekelezaji wa miradi ya kupeleka umeme vijijini kwa nchi nzima kwa kupeleka umeme katika vijiji ambavyo havijafikiwa na umeme.

Mheshimiwa Spika, vijiji tisa vya Jimbo la Nsimbo ambavyo havina umeme ikiwa ni pamoja na Vijiji vya Kata ya Ugalla vya Katambike, Mnyamasi na Kasisi vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu mzunguko wa pili unaoendelea. Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Machi, 2021 na unatarajiwa kukamilika Desemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo inahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33, urefu wa kilomita 63.6; msongo wa kilovoti 0.4, urefu wa kilomita 3.0; na ufungwaji wa transfoma tatu, pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali zaidi ya 66. Gharama ya mradi ni Shilingi bilioni 2.46.