Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Irene Alex Ndyamkama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. IRENE A. NDYAMKAMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakarabati Meli ya Mv. Liemba pamoja na kujenga meli mpya ambazo zitachochea ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Rukwa?

Supplementary Question 1

MHE. IRENE A. NDYAMKAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa meli hii imedumu takribani miaka 100 na ilikuwa mkombozi wa Wana-Ziwa Tanganyika, nikimaanisha Rukwa, Katavi na Kigoma. Je, ni lini sasa Serikali itakarabati meli hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Ziwa Tanganyika lina uchumi mkubwa na Serikali imetujengea bandari mbili, Bandari ya Kasanga na Bandari ya Kabwe. Ni lini Serikali itatujengea meli mpya Mkoa wa Rukwa kama mikoa mingine ili wananchi wa Mkoa wa Rukwa wafaidike na Serikali yao? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, asante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Irene Ndyamkama, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi ni kwamba, tayari Mv. Liemba ipo kwenye hatua nzuri kwa sababu mkandarasi amekwishapatikana na mwezi ujao tuna-sign mkataba ili kazi iendelee. Kwa hiyo, katika hili la Mv. Liemba kama ambavyo Wabunge wengi wa Mkoa wa Katavi na maeneo ya jirani walizungumza wakati wa bajeti, tumezingatia linafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili tumepokea hoja yake ya kupata meli ya Mkoa wa Katavi kama mikoa mingine. Tutalifanyia kazi kadiri ambavyo Serikali itapata fedha za kutekeleza hilo, ahsante.