Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza:- Je, ni sheria ipi ambayo ilitumika kuchukua ardhi ya Mlima Nkongore kutoka kwa wananchi na kulipatia Jeshi la Magereza?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii kuuliza swali la nyongeza.

Ningependa kujua, kwasababu wamesema kwamba wananchi wale ambao walikuwa wanalima katika mlima ule walikuwa wanaharibu mazingira na bado magereza ambao wanapewa eneo lile wameendeleza kilimo kama walivyokuwa wanafanya wananchi. Sasa ningependa kujua kilimo cha wale waliopewa Magereza wao hawaharibu mazingira au wananchi ndio wanaharibu mazingira?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ningependa kujua kama Mlima Nkongole ndio pekee ambao Serikali imeona kwamba uhifadhi lakini ukienda maeneo kama Mwanza wananchi wanaishi mlimani.

Je, ni mlima Nkongole peke yake ndiyo imeonekana ni hifadhi au iutumie au kwa milima yote ambayo ipo katika nchi hii ndiyo inayohifadhiwa na Serikali? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita, Mbunge wa Tarime Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, ajenda ya uharibifu wa mazingira, haijalishi mtu ama taasisi kama watu binafsi wanaharibu mazingira, kama Jeshi la Magereza linaharibu mazingira ama taasisi yoyote inaharibu mazingira wote ni waharibifu wa mazingira. Kwa haina excuse ya aina yoyote na kutokana na jibu la msingi Naibu Waziri, Ofisi ya Rais - TAMISEMI alivyokuwa akijibu hapa alieleza wazi kama eneo hilo lipo katika mchakato katika maeneo lindwa. Sio eneo hilo peke yake, isipokuwa kuna maeneo mengine ya fukwe na maeneo mengine ambayo sisi Serikali tumeona kwamba kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 sasa kuna mchakato wa kuainisha maeneo hayo yote.

Kwa hiyo, tuseme kama Jeshi la Magereza licha ya kukabidhiwa wanaharibu mazingira maana yake jambo hilo halifai na ofisi yetu inasema jambo hilo tutaendelea kulisimamia kwa karibu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa nini maeneo mengine watu bado wanaendelea kujenga nyumba. Tumesema sasa hivi tutakuwa nimetoa maelekezo mahasus katika upande wa mazingira na ndio maana katika suala zima ambalo tutalizindua siku ya tarehe 5 Juni, 2021 Kampeni Kabambe ya Kimazingira miongoni mwa mambo hayo tutakayokwenda kuyaainisha ni suala zima la utoaji elimu katika suala zima la utunzaji wa mazingira.

Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge sote tushirikiane pamoja katika ajenda kubwa ya kulinda mazingira hususan kuilinda nchi yetu. Ahsante sana. (Makofi)