Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, kwanza naanza kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri kwa kuitangaza hifadhi yetu ya Taifa ya Katavi lakini nina maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Swali la kwanza ilikuwa ni ahadi ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, mwaka 2019 ya kujenga hoteli ya Kitalii katika Mkoa wa Katavi katika Kata ya Magamba, ili hoteli hiyo iweze kuwavutia zaidi watalii kwa kupata malazi yaliyo bora na malazi yanayoridhisha. Je, huo mpango wa kujenga Hoteli ya kitalii katika Kata ya Magamba ambapo tulishatenga eneo umefikia wapi Ukizingatia hoteli hii itakwenda kuibua fursa nyingi kwa vijana wanaozunguka katika Mkoa wa Katavi kuweza kuapta ajira? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili vijiji vinavyozunguka hifadhi ya Taifa ya Katavi vikiwepo vijiji vya Mwamapuri, Chamalindi, Ikuba, Starike, Mangimoto, na Kibaoni vijiji hivi kwa muda mrefu vimekuwa havinufaiki na ujirani mwema kwa kupata miradi ya maendeleo kupitia TANAPA. Je, Serikali inatoa tamko gani ili vijiji hivi viweze kunufaika na hifadhi hiyo ukizingatia vijiji hivyo ndivyo vinavyotunza hifadhi hiyo? Ahsante. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martha Maliki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la hoteli ya kitalii kujengwa katika hifadhi ya Katavi ni kweli Hayati Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, aliahidi katika ziara zake kwamba kujengwe hoteli ya kitalii katika hifadhi ya Taifa ya Katavi. Mpango huo umeshapangwa na kwenye mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022 mpango huu tumeuweka na hoteli hii ya kitaifa itaanza kutekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuhusu ujirani mwema, ujirani mwema ni kweli Serikali imekuwa ikisaidia vijiji vyote vinavyozunguka maeneo ya hifadhi ikiwemo hifadhi ya Taifa ya Katavi lakini kwa mwaka wa fedha 2021 tulikuwa na changamoto ya Korona hivyo tulishindwa kuhudumia haya maeneo ya hifadhi kama ambavyo Serikali imekuwa ikipanga. Lakini nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili sasa tunaenda kulitekeleza katika mpango wa fedha wa mwaka 2021/2022 vijiji vyote vinavyozunguka hifadhi za Taifa, ujirani mwema utaenda kutekelezwa kwa kiwango cha juu, ahsante, (Makofi)

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Serikali ina mpango gani wa kuutangaza utalii wa ndani kwa kutumia Wabunge pamoja na Halmashauri zetu? Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana nimpongeze Mheshimia Asia kwa swali lake hilo zuri pia nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango mkakati kabisa wa kushirikiana na Halmashauri zote na Serikali za Mikoa na Wilaya katika kutangaza Utalii ikiwemo kuwatumia Wabunge pia katika kutangaza utalii. Ni wazi umeona tayari Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na baadhi ya Wabunge tumeshaanza kushirikiana nao kuhakikisha kwamba tunatangaza utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiongezea kwenye majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwamba maelekezo ya Mheshimiwa Hayati Dkt. Magufuli yalikuwa ni kwamba tupunguze gharama za utalii ili kuwezesha Watanzania wengi zaidi na watalii wengi zaidi kwenda kwenye sehemu za vivutio vya Utalii, zoezi hili tumeshalianza tunaamini gharama hizo zitashuka na Watanzania waweze kufaidi maliasili zao. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa Katavi?

Supplementary Question 3

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kwa kuwa utalii unakwenda kwa package na mbuga ya Katavi pamoja na hifadhi nyingine ni sehemu ya utalii kusini na kituo cha utangazaji na taarifa zote kinatakiwa kujengwa Iringa katika sehemu inayoitwa Kisekiroro ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa kituo hicho unafadhiliwa na Benki ya Dunia katika Mradi wa RIGRO. Mradi huo ulichelewa kidogo kutokana na tatizo la COVID ambalo liliwakuta nchi mbalimbali ikiwemo wafadhili wa Mradi huo. Sasa hivi tayari mradi huo umeshaanza, jana Katibu Mkuu amekabidhi magari 12 kutokana na mradi huo kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Jesca na Wabunge wote wa Iringa na Nyanda za Juu Kusini kwamba kituo hicho kitajengwa haraka iwezekanavyo.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa Katavi?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana Mheshimiwa Rais alipokuja Mkoa wa Katavi aliagiza Wizara ya Maliasili na Wizara ya Ardhi kumaliza tatizo la migogoro ya ardhi kati ya mapori ya akiba na hifadhi ya Taifa ya Katavi. Lakini utekelezaji mpaka sasa bado haujafanyika ni lini Mheshimiwa Waziri atakuja Mkoa wa Katavi ili asimamie zoezi hili?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Katavi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya Bunge hili Tukufu tutaongozana naye kwenda kutatua taizo hili kwa hiyo nimuondoe wasiwasi tutaondoka naye, ahsante. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa Katavi?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa kuuliza swali la nyongeza. Ni dhahiri kwamba kwa Afrika nchi yetu inahifadhi nzuri inawanyama wengi ukienda Ruaha ukienda Serengeti, Ukienda Tarangire na maeneo mengineā€¦

MWENYEKITI: Mheshimiwa Bulaya ukipewa swali la nyongeza usianza na utaalam mwingi nenda straight to the question.

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mikakati ya Serikali ni ile ile ya kushiriki matamasha ya Kimataifa, kutangaza kwenye TV lakini bado hayajatuletea manufaa chanya ya ongezeko la watalii kulingana na vivutio vyetu na hifadhi zetu.

Je, hamuoni kwamba ni wakati muafaka wa kuwa na mikakati Madhubuti ya kiushindani ili idadi ya watalii iendane na hifadhi zetu na vivutio vyetu? (Makofi)

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nimshukuru Mheshimiwa Ester Bulaya kwa swali lake hilo, takwimu zetu zimeonesha kwamba idadi ya watalii imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Ongezeko hilo limetokana na juhudi ya Serikali ambayo imeifanya katika kutangaza utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Ilani ya Chama Cha Mapinduzi imeelekeza wazi kwamba tuje na mazao mapya na mikakati mipya katika kutangaza utalii, mikakati yote ipo mezani iko tayari kinachotukwamisha ni gonjwa hili la Covid, nimhakikishie Mheshimiwa Ester Bulaya pindi ugonjwa huu utakapokwisha ataona ongezeko kubwa la watalii hapa Tanzania, ahsante. (Makofi)