Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Maswa hadi Lalago?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, swali la kwanza, ni jepesi tu; ni lini ujenzi unaanza, basi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kama Serikali ya Ujerumani imeweza kutoa fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu, inakuwaje Serikali inasuasua kutoa fedha kwa ajili ya usanifu wa kina? Hivi hata hao wanatoa fedha za ufadhili katika hatua hizi za awali hatuoni kama tunawa-discourage kwa kitendo cha Serikali kusuasua kutoa fedha za kuendeleza mradi huu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni hayo tu.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nimesema barabara hii itaanza mara fedha itakapopatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimhakikishie katika swali lake la pili, kuhusu kwamba Serikali inasuasua. Kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi hii Barabara inapita Maswa – Lalago – Mwanhuzi – Sibiti – Hydom – Mbulu – Karatu. Katika baadhi ya barabara, hii tayari kama mlivyosikia jana kwenye bajeti, kipande cha Mbulu – Haidom kitaanza kujengwa. Pia Mheshimiwa Waziri jana amesema barabara hii itatangazwa siku za karibuni ambayo ni sehemu ya hii barabara kwa fedha za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, hata hicho kipande ambacho sasa tutafanya ni design and build, yaani ni kufanya usanifu na ujenzi, basi hela ikipatikana hata kipande hiki cha Lalago – Maswa kitajengwa. Ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Maswa hadi Lalago?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Changamoto zilizoko Maswa Mashariki kuhusu barabara zinafanana sana na changamoto ambazo ziko Arumeru Mashariki. Kuna barabara inayoanzia Tengeru kwenda Mererani, inaunganisha Mkoa wa Arusha na Manyara, lakini pia ni kiungo muhimu kwa shughuli za uchimbaji Mererani na soko ambalo liko Mjini Arusha. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara hii ni muhimu sana na Mheshimiwa Pallangyo amekuwa akiifuatilia sana, lakini bado tunasema nia ya Serikali ni kujenga hizi barabara ambazo zimeainishwa na zinarahisisha maisha ya wananchi kama zitajengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Pallangyo, Serikali inaendelea kutafuta fedha na fedha ikipatikana basi hii Barabara ya Tengeru kwenda Mererani, sehemu ambayo kuna machimbo ya tanzanite itajengwa ili kuweza kuboresha maisha na kupandisha uchumi, lakini pia kurahisisha biashara ya tanzanite kule Arusha. Ahsante.