Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 31 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 267 2021-05-19

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Maswa hadi Lalago?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroun Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Maswa – Lalago yenye urefu wa kilometa 34 ni barabara ya mkoa inayohudumiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Barabara hii ni sehemu ya Mradi wa Serengeti Southern by-pass ikianzia Maswa – Lalago – Mwanhuzi – Sibiti hadi Karatu yenye urefu wa kilometa 338. Mradi huu ulihusisha kazi ya Upembuzi Yakinifu chini ya ufadhili wa Serikali ya Ujerumani na umeshakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza usanifu wa kina na ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Aidha, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali sehemu hii ya Maswa – Lalago na inapitika majira yote ya mwaka. Ahsante.