Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE K.n.y. MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi na kuanza kutumia Hospitali ya Wilaya ya Mufindi?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nataka niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja, hospitali hiyo iko mbali na makazi ya watu, ni upi mpango wa Serikali sasa katika kujenga makazi kwa ajili ya watumishi wa hospitali hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, ni upi mpango wa Serikali katika kutatua kero kubwa ya wataalam wa sekta ya afya katika zahanati na vituo vya afya vilivyopo katika Jimbo letu la Mufindi Kusini? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya Mheshimiwa David Kihenzile, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameuliza hapa ni lini Serikali itajenga makazi kwa ajili ya watumishi wa afya wa Hospitali ya Halmashauri ya Mufindi. Nimueleze tu kwamba katika jitihada za Serikali, moja ya jitihada kubwa ni kama tulivyoeleza katika jibu letu la msingi tumekuwa tukiongeza fedha kuhakikisha tunaboresha hospitali hiyo na kila mwaka tumekuwa tukitenga fedha. Kwa hiyo, nimueleze tu kwamba tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo kuanzia wodi, OPD pamoja na nyumba za watumishi kadri ya upatikanaji wa fedha. Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi, Serikali ina nia njema kwenye suala hili na tutalifanyia kazi ombi lake na siyo tu kwa Hospitali ya Wilaya ya Mufindi bali kwa nchi nzima katika vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili kuhusiana na kero ya wataalam, Serikali inaendelea na ajira na katika kipindi hiki Serikali itaajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya zaidi ya 2,600. Katika mgawanyo huo, sehemu ya watumishi hao tutawapeleka katika Halmshauri ya Wilaya ya Mufindi kwa ajili ya kupangwa kwenye vituo vyake vya afya. Ahsante sana.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE K.n.y. MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi na kuanza kutumia Hospitali ya Wilaya ya Mufindi?

Supplementary Question 2

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa changamoto zilizoko katika swali la msingi ni sawa na zilizoko katika Jimbo langu la Kinondoni katika Kata ya Makumbusho ambako kuna dispensary ilianza kujengwa tangu mwaka 2019 na ilikuwa imalizike Aprili, 2020, sasa hivi ni mwaka mmoja haijamalizika.

Pamoja na juhudi za Manispaa kusimamia ujenzi ule na Mfuko wa Jimbo, je, Serikali haiwezi ikatia mkono sasa kuhakikisha kwamba dispensary ile inamalizika ili wananchi wa Kata ya Makumbusho, Jimbo la Kinondoni waweze kupata huduma? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza Mheshimiwa Abbas Tarimba, Mbunge wa Kinondoni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameiomba Serikali kuweka mkono katika Kata ya Makumbusho kwenye eneo ambalo limejengwa dispensary ambayo ilikuwa imepaswa kumalizika Aprili, 2020. Tunatambua jitihada kubwa zinazofanywa na Halmashauri ya Kinondoni hususan katika sekta ya afya, tunatambua kazi kubwa anayofanya Mbunge katika Jimbo la Kinondoni na tunatambua kazi nzuri inayofanywa na Serikali kuboresha sekta ya afya nchini.

Kwa hiyo, tumelipokea ombi lake lakini tutaendelea kusisitiza Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni sisi pamoja na wao kwa pamoja tuimalize dispensary hii ili wananchi waanze kupata huduma za afya.