Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Je, mpango wa Serikali wa ujenzi wa uwanja wa ndege eneo la Kisumba, Wilayani Kalambo umefikia hatua gani kwa sasa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru pamoja na majibu ya Serikali naomba niulize maswali madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; hii hadithi ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege Sumbawanga ni hadithi ya muda mrefu na wananchi wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu. Sasa naomba kupata majibu ya Serikali ni nini ambacho kinakwamisha upatikanaji wa fedha kwa sababu tumekuwa tukisubiri muda mrefu ili ujenzi huu uanze mara moja? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa sababu ujenzi wa uwanja ulioko Sumbawanga uko katikati ya Mji na kwa kuliona hilo Serikali iliamua kwa makusudi mazima kutenga eneo lingine na si kama airstrip kama ambavyo Naibu Waziri amejibu. Aliyekuwa Makamu wa Rais Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Dkt. Ghalib Bilal alifika eneo la Kalambo na kuweka jiwe la msingi ili eneo lile liendelee kulindwa. Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuhakikisha kwamba eneo lile halivamiwi ili itakapofika wakati wa kujenga uwanja mkubwa kusiwe na haja ya fidia? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Kandege, Mbunge wa Kalambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyotoa maelezo yangu kwenye jibu la msingi ni kwamba jambo hili linafanyiwa kazi na Mheshimiwa Kandege anafahamu taratibu za Serikali, kama jambo ni makubaliano ya kimkataba lazima yakamilike. Hata hivyo, nipokee hoja yake kama kweli kuna ucheleweshaji tutalifanyia kazi ili uwanja huu ukamilike kama ambavyo tumeahidi kwenye jibu letu hapa kwa niaba ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nipokee ushauri wake wa pili kwamba eneo hili ni kweli kwamba juzi nilikuwa Mtwara, hoja mojawapo iliyopo kule ni kwamba wananchi wamesogea karibu na eneo na wahitaji kulipwa fidia ambayo ni gharama nyingine kubwa tena kwa Serikali. Eneo hili litasimamiwa, lipimwe liwekwe mipaka na vizuizi ili libaki kwa matumizi ambayo limekusudiwa na wananchi wasianze kugombana na Serikali kwa kudai fidia ambayo itaongeza gharama pia katika maeneo hayo. Ahsante.