Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 28 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 238 2021-05-12

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-

Je, mpango wa Serikali wa ujenzi wa uwanja wa ndege eneo la Kisumba, Wilayani Kalambo umefikia hatua gani kwa sasa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa sasa imejikita katika kukamilisha ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga kilichopo Mkoani Rukwa ambacho ni miongoni mwa Viwanja vya Ndege vinne (4) vilivyofanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kupata ufadhili kutoka Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank - EIB). Aidha, Serikali imekamilisha taratibu za kupata Mkandarasi na kupewa Idhini (No Objection) kutoka EIB, kinachosubiriwa ni kupata fedha baada ya taratibu za kimkataba kukamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumfahamisha Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege kwamba, baada ya Serikali kukamilisha Ujenzi wa Viwanja vya Ndege vya mikoa vilivyosalia ikiwemo Sumbawanga, Serikali itaendelea na ujenzi wa viwanja vidogo vya ndege kwa hadhi ya airstrip ikiwa ni pamoja na Kiwanja cha Ndege cha Kalambo.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwashauri wananchi wa Kalambo kutumia Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga mara ujenzi wake utakapokamilika.