Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Je, ni upi mpaka sahihi wa Bonde la Kilombero kati ya mpaka uliowekwa mwaka 2012 na ule uliowekwa mwaka 2017?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi hawa wanaelewa lakini suala hili limechukua muda mrefu, walikuwa wanatumia maeneo haya kulima na wanajua faida ya Bwawa la Mwalimu Nyerere lakini wanachohitaji ni kupata uelewa na kufahamishwa. Kwa kuwa Mawaziri wameshapitisha na suluhisho limeishafikiwa, je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakwenda kuongea na wananchi hawa kusudi waweze kupata suluhisho? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, tatizo hili lipo pia katika Kitongoji cha Dutumi, Kata ya Bwakila Chini, Wilaya ya Morogoro Vijijini ambapo kuna tatizo la Hifadhi ya Selous pamoja na wananchi wa Dutumi hasa wakiwemo wakulima na wafugaji kiasi kwamba kuna kijana mmoja alitobolewa macho, mwingine amejeruhiwa mkono, ni lini Mheshimiwa Waziri atakwenda kuwasikiliza kwa sababu vikao vimekaa lakini hakuna suluhisho? Ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kabla ya bajeti hii kuisha Juni tutaongozana naye kwenda Kilombero lakini pia Morogoro Vijijini ili kutatua mgogoro huu wa wakulima na wafugaji.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Je, ni upi mpaka sahihi wa Bonde la Kilombero kati ya mpaka uliowekwa mwaka 2012 na ule uliowekwa mwaka 2017?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa hawa wanyamapori wamekuwa wakivamia vijiji na kushambulia wananchi hususan Wilaya ya Nyang’wale zaidi ya wananchi 10 wameliwa na fisi. Je, Serikali ina mpango gani wa kwenda kuwatembelea na kuwapa pole lakini pia kuwalipa kifuta machozi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyang’wale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kumpa pole sana Mbunge wa Nyang’wale na Wabunge wengine wote ambao wamekumbana na athari hii. Nimhakikishie kwamba hawa fisi ambao wako kwenye maeneo ya Nyang’wale na maeneo mengine yote yanayoathiriwa na wanyama hawa tutaenda kuwahamisha na tutawarudisha hifadhini, kwa sababu Nyang’wale ni eneo ambalo kidogo hifadhi ziko mbali na makazi ya wananchi lakini fisi wanaendelea kwenda kwenye maeneo hayo. Pia tutaongozana naye kwenda kuwaona wananchi hao na tutashirikiana kadri itakavyowezekana.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Je, ni upi mpaka sahihi wa Bonde la Kilombero kati ya mpaka uliowekwa mwaka 2012 na ule uliowekwa mwaka 2017?

Supplementary Question 3

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa masuala haya ya mipaka baina ya makazi ya watu na maliasili yamekuwa ni ya kudumu lakini nchi hii inaongozwa na sheria, Sheria Sura 324 inampa Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani mamlaka ya kuhakiki mipaka pale panapotokea mgogoro. Kule kwenye Jimbo la Ukonga upo mgogoro mkubwa baina ya Msitu wa Kazimzumbwi na wananchi wa Kata za Buyuni, Chanika na Zingiziwa. Tayari uhakiki ulifanyika tarehe 24 Februari, 2012 na magazeti yote yalitoa tangazo na lipo linafahamika.

Je, ni lini Waziri atakuwa tayari tuambatane na wataalam wa Wizara ya Ardhi kwenda kuhakiki mpaka huu na kuwaondolea kero ya kupigwa, kubakwa na kuchukuliwa hatua kinyume na sheria wananchi Jimbo la Ukonga?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mbunge Jerry Silaa kwa kuendelea kuwaonyesha wananchi wake kwamba wamemtuma kwa kazi maalum hapa Bungeni. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya bajeti hii tutaongozana naye kwenda kutatua mgogoro huu. Ahsante.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Je, ni upi mpaka sahihi wa Bonde la Kilombero kati ya mpaka uliowekwa mwaka 2012 na ule uliowekwa mwaka 2017?

Supplementary Question 4

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji vyangu vya Ndaleta, Ngabolo, Olkoponi, Pori kwa Pori, Mbeli, Amei, Namelok wanasumbuliwa sana na tembo na hivi tunavyozungumza tembo wako mashambani. Nini kauli ya Serikali kwa wananchi hawa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Olelekaita, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee kutoa pole kwa wananchi wanaozunguka maeneo hayo, lakini Serikali kama ambavyo nilisema mwanzo kwamba tumeanza kutoa mafunzo baada ya kuona athari hii inaendelea kuongezeka. Mafunzo haya yatatolewa nchi nzima namna ya kukabiliana na hawa wanyama wakali. Pia tutatoa vifaa maalum kwa ajili ya kudhibiti hawa wanyama wakali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana pale ambapo inatokea watupe taarifa na vikosi kazi ambavyo tumevisambaza nchi nzima vitaendelea kufanya kazi kudhibiti hawa wanyama wakali.