Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 26 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 223 2021-05-10

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:-

Je, ni upi mpaka sahihi wa Bonde la Kilombero kati ya mpaka uliowekwa mwaka 2012 na ule uliowekwa mwaka 2017?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Pori Tengefu la Kilombero (Kilombero Game Controlled Area) lilianzishwa kupitia Tangazo la Serikali (GN) Na. 107 chini ya Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori na Mimea (Fauna and Flora Ordinance) ya Mwaka 1951 iliyoanza kutumika mwaka 1952. Baada ya kurejea mwaka 1974, Pori Tengefu la Kilombero lilitambulika kwa GN. Na. 269 ya mwaka 1974 iliyohuishwa kwa GN. Na. 459 ya Mwaka 1997 chini ya Sheria ya Wanyamapori Na. 12 ya mwaka 1974 lilikuwa na ukubwa wa kilomita za mraba 6,500. Pori hilo ni sehemu ya ardhioevu ya Bonde la Kilombero lenye ukubwa wa kilometa za mraba 7,950. Aidha, bonde hilo linachangia takriban asilimia 62.5 ya maji yote ya Mradi wa Bwawa la Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere.

Mheshimiwa Naibu Spika, Pori Tengefu Kilombero halijawahi kubadilishwa mipaka yake. Hata hivyo, mwaka 2012 na 2017 iliwekwa alama kwa ajili ya kuokoa kiini cha Mto Kilombero. Aidha, Serikali iliunda Kamati ya Mawaziri Nane (8) kwa ajili ya kushughulikia migogoro ya ardhi ya maeneo yaliyohifadhiwa na watumiaji wengine wa ardhi likiwemo Bonde hilo la Mto Kilombero. Kamati hii ilitoa mapendekezo ambayo yalijadiliwa kwenye Baraza la Mawaziri na maamuzi yake yamekwishafanyika na utekelezaji wake utatolewa hivi karibuni.