Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo – Kilosa kwa Mpepo, inayounganisha mkoa wa Ruvuma na Morogoro kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali iliona umuhimu wa kujenga barabara hii na barabara hii ni ya kimkakati dhidi ya masuala ya kiuchumi ambayo inakwenda kujengwa kwa ajili ya kuinua uchumi wa Kikanda, Kimkoa na Kitaifa, na barabara hii ilishafanyiwa upembuzi wa kina na upembuzi huo ulishakamilika toka mwaka 2018. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kupeleka huko kwa ajili ya kuana ujenzi huo haraka iwezekanavyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ucheleweshaji wa ujenzi wa barabara hii ya kimkakati ambao unachukua muda mrefu sana kuanza kujengwa je, Serikali haioni kwamba kutokuanza kujenga barabara hii kwa haraka inaendelea kusababisha udumavu wa ukuaji wa uchumi katika Mkoa wa Ruvuma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ina urefu wa kilometa 521 kwa hiyo ni uwekezaji mkubwa na tayari tulishaanza jitihada za kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami kwa hatua za awali ikiwa ni pamoja na hizo hatua ambazo tayari zimeshafanyika usanifu wa kina lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Msongozi kwamba tayari tumeshaanza ujenzi wa kiwango cha lami katika vipande kadhaa ambavyo nimevitaja ikiwa ni pamoja na ujenzi wa kiwango cha lami kilometa 66.9 kuanzia Kidatu kwenda Ifakara, na bado tumehakikisha kwamba barabara hii itakwenda kutengenezwa kadri fedha zitakapokamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nia ya Serikali ni kuikamilisha barabara hii ili kuifungua Ruvuma na kanda yote ya kusini ambayo inatumia barabara hii. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kadri fedha zitakapoendelea kupatikana barabara hii tutahakikisha tunaiunganisha kwa Mikoa ya Ruvuma na Morogoro kupitia kwenye hiyo barabara ambayo amesema ambayo inapita kwenye mbuga za Selous na ni miinuko mikali kwa hiyo, uwekezaji ni mkubwa lakini Serikali inatafuta fedha na tunahakikisha tutaijenga, ahsante.

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo – Kilosa kwa Mpepo, inayounganisha mkoa wa Ruvuma na Morogoro kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii kuuliza swali, swali langu ni kwamba mwezi mmoja uliopita daraja lilikatika katika mji wetu wa Tarime na likasababisha vifo vya watu watatu na wengine watatu mpaka sasa hivi hawapatikani na inadhaniwa kwamba walikwenda na maji, na hata sasa hivi ninavyozungumza kuna daraja limekatika kipande kimoja daraja ambalo linatoka mjini kuelekeza Kibaga ambako wanachimba madini na kuna magari makubwa yanabeba makinikia yanapita pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba je, ni lini watarekebisha hili daraja ili lisije likaleta maafa mengine kama ilivyosababishwa na kuvunjika kwa daraja, ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine kwamba Serikali inatambua kwamba mwaka huu kumekuwa na uharibifu mkubwa sana wa barabara nyingi na hasa hizi za changarawe na udongo. Na sisi kama Wizara tulishalitambua hilo tuna maandalizi ambayo tulishayafanya ikiwa ni pamoja na kununua madaraja ya dharula lakini imekuwa ni vigumu sasa hivi kutengeneza hizo barabara kwasababu nyingi sio tu zinahitaji kuweka madaraja lakini pia zinahitaji kuweka matuta ambayo yanainuliwa sasa inakuwa ni ngumu kufanya kazi hiyo katika kipindi hiki ambacho mvua inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine kwamba barabara zote inaainishwa zile ambazo zimepata changamoto hasa kutokana na mvua na mara hali ya hewa itakapokuwa vizuri wakandarasi wapo tayari watazirejesha barabara hizi zote katika hali yake ya kawaida ili ziendelee kutumika ikiwa ni pamoja na barabara ya Mheshimiwa Michael Kembaki Mbunge wa Tarime.

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo – Kilosa kwa Mpepo, inayounganisha mkoa wa Ruvuma na Morogoro kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kuniona hali ya barabara ya Lumecha kilosa inafanana kabisa na ile ya Bungwi Nyamisati je, ni lini sasa Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami ikizingatiwa ni muhimu kwa wananchi wa Mafia, Mkuranga na Kibiti yenyewe? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri barabara ya Bungwi Nyamisati nimefika na tukiwa tumeongozana na Mheshimiwa Mbunge Mpembenwe naomba nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba hii ni barabara ambayo ni ahadi ya viongozi wa Kitaifa lakini pia ipo kwenye Ilani ambayo inaunganisha wananchi wa Mafia na wanaokuja bara, kwa hiyo ipo kwenye mpango, fedha itakapopatikana barabara hii itajengwa ili kuifanya wananchi waweze kupata huduma bora ya barabara, ahsante. (Makofi)

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo – Kilosa kwa Mpepo, inayounganisha mkoa wa Ruvuma na Morogoro kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali iliahidi babarara ya Njiapanda Mang’ola, Matala Mwausi Lalago, kwa kiwango cha lami kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi sasa ni lini bararara hiyo itajengwa kwa kiwango cha Lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, tunategemea kupitisha ama kuleta bajeti yetu ili iweze kujadiliwa naomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira ili kipindi cha bajeti tutaitolea maelezo sahihi kuhusu hiyo barabara ambayo ameisema na nimhakikishie tu kama nilivyosema kwenye majibu mengine ya msingi na wananchi wa Jimbo lake kwamba barabara ambazo zote zimeahidiwa na kuwa kwenye Ilani zipo kwenye mpango wa Kipindi cha Miaka Mitano na tutazijenga kadri ya fedha zitakapoendelea kupatikana. Ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo – Kilosa kwa Mpepo, inayounganisha mkoa wa Ruvuma na Morogoro kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara ya Loliondo – Wasu - Mto wa Mbu ni ahadi ya muda mrefu kwamba barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami. Natambua kuna kipande cha Waso - Sale kilometa 49 sasa hivi kinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami ila kuna eneo korofi sana la Sale – Ngaraesero, je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupitia Bunge lako nimuagize Meneja wa TANROADS Mkoa aweze kwenda kwenye barabara hii ya Sale - Ngaraesero ili aweze kufanya tathmini na aone kama tunaweza tukajenga kipande; imekuwa ni kawaida sehemu ambayo tunaona ni korofi yenye vilima ama yenye miteremko mikali ama yenye utelezi aende akafanye tathmini na kuleta bajeti ili tuone namna ambavyo tunaweza tukafanya ili tusikwamishe wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Mheshimiwa awe na amani na ikiwezekana baada ya kikao hiki tuweze kukutana ili aweze kunipa taarifa kamili ya eneo hilo ili tuweze kulifanyia kazi. Ahsante.