Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kairuki hadi Mikocheni Shoppers ambayo hadi sasa imejengwa kipande kidogo?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niseme kwamba katika Jimbo la Kawe kuna barabara kama hizo ambazo ni sugu kama Barabara ya Ununio – Malindi, Mbweni – Teta mpaka Mpiji. Barabara hii inajengwa lakini inasuasua kwa muda mrefu: Ni lini sasa Serikali itamalizia barabara hii ili wananchi hawa waweze kupata nafuu?

Swali la pili, ni mkakati gani endelevu wa Serikali ambao sasa baada ya barabara hizi kujengwa wataweka mitaro ambayo haitaathiri barabara hizi kwa sababu imeonekana barabara nyingi zinaharibika kwa sababu ya mitaro? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Mbunge amejaribu kuainisha baraba nyingine katika Jimbo la Kawe ambazo ni mbovu ikiwemo barabara ya Ununio – Malindi, Mbweni – Teta mpaka Mpiji na akaiomba Serikali izitengeneze. Najua Mheshimiwa Mbunge anafanya kazi nzuri na mimi nimwahidi kabisa kwamba kama tulivyozungumza katika swali letu la msingi, tutaendelea kufanya tathmini na kadri tutakavyopata fedha hizo barabara zitatengenezwa. Hiyo ndiyo nia ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na mama yetu Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili amejaribu kuainisha kwamba ni mkakati gani ambao unaweza kusaidia zile barabara zetu zisiharibike ikiwemo kujenga mitaro itakayopitisha maji nyakati za mvua? Hata hivyo, Mheshimiwa Mbunge anatambua kabisa kwamba kuna mpango mkubwa wa DMDP wa ujenzi wa barabara kwa maana ya miundombinu yote katika Jiji la Dar es Salaam. Sehemu ya fedha ambazo zipo ni pamoja na kujenga mitaro ili kuhakikisha barabara zetu zote zinakuwa na ubora katika muda wote. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie mkakati wa Serikali ni pamoja na kuendelea kujenga mitaro, madaraja na kuziboresha barabara zetu kwa kipindi chote. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kairuki hadi Mikocheni Shoppers ambayo hadi sasa imejengwa kipande kidogo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa changamoto ya Barabara ya Kairuki ni sawa kabisa na changamoto iliyopo katika barabara ya kutoka Ndala kwenda Mwawaza kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kukamilisha barabara hiyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Christina Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameainisha Barabara ya Ndala – Mwawaza kuelekea Hospitali ya Shinyanga. Ameuliza ni lini Serikali itaikamilisha. Niseme tu kwamba, tutaikamilisha kwa kadri ya upatikanaji wa fedha na tathmini ambazo zinaendelea kufanyika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge awe na subira, hiyo barabara itajengwa kwa kadri tutakavyopata fedha. Ahsante sana.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kairuki hadi Mikocheni Shoppers ambayo hadi sasa imejengwa kipande kidogo?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa, ndani ya Jimbo la Kibamba ipo barabara ya Temboni – Msingwa kwenda Kinyerezi ina changamoto kubwa sana kwa muda mrefu. Je, mchakato unaoendelea kupata mkandarasi ni lini utakamilika na barabara hiyo kuanza kujengwa chini ya TARURA?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Issa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameainisha kwamba, barabara ya Temboni – Msimbwa kwenda Kinyerezi imeharibika na anataka kujua lini barabara hii itaanza kujengwa. Nimwambie tu kwamba, mchakato unaendelea na mchakato utakapokamilika kama ambavyo yeye ameainisha, tutakapomaliza huu mchakato hii barabara itaanza kujengwa mara moja kwa sababu, tumeshaitenga katika bajeti. Ahsante sana.