Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 217 2021-05-10

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kairuki hadi Mikocheni Shoppers ambayo hadi sasa imejengwa kipande kidogo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratias Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Kairuki hadi Mikocheni Shoppers inayojulikana kwa jina la Barabara ya Warioba - Chakwu yenye urefu wa kilomita 1.73 ilijengwa kwa kiwango cha lami kipande cha kilometa 1.13 kwa gharama ya shilingi bilioni 1.017 katika mwaka wa fedha 2014/2015. Hivyo, kipande chenye urefu wa kilomita 0.6 hakikujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii yote inahitaji matengenezo makubwa kikiwemo kipande cha kilometa 0.6 ambacho hakina lami. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 TARURA Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imepanga kufanya tathmini ya barabara hii na Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kujenga na kuifanyia matengenezo barabara hii kwa mujibu wa matokeo ya tathmini.