Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWEL X. HHAYUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya Kondoa – Gisambalang – Nangwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWEL X. HHAYUMA: Ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali yenye kutia matumaini, nina maswali mawili madogo. Swali la kwanza; kwa kuwa barabara hii inategemewa na wananchi, upande wa Hanang’ tu zaidi ya 100,000 wa Kata za Gisambalang, Bilmaa, Simbai, Isilo, Wareta na Nangwa yenyewe na kulikuwa na Daraja la Mungurwi B. Daraja lile limechukuliwa na mafuriko ya mvua iliyonyesha 2019/2020. Ni kwa nini Serikali daraja lile lilivyochukuliwa halikuwekwa kwenye mpango wa dharura wa kulirudishia?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa daraja lile la Mto Bubu limekuwa likigharimu Maisha ya watu na kupoteza mali kwa kusombwa na maji. Je, Serikali ina mpango gani wa dharulra ili kuhakikisha wananchi wanaendelea na shughuli zao za kijamii pamoja na biashara? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Samwel Hhayuma, Mbunge wa Hanang’, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba daraja la Mungurwi B lilisombwa na maji na ni daraja ambalo liko sehemu ya bonde ambapo baada ya kusombwa lilitengeneza umbali wa mita zaidi ya 200 na hivyo ilikuwa ni ngumu sana kulijenga kama lilivyokuwa na badala yake, daraja hili linafanyiwa usanifu kutoka ilipokuwa kupanda eneo la juu ambalo tunaamini litakuwa ni eneo fupi, lakini pia hakutakuwa na changamoto ya mafuriko. Kwa hiyo linafanyiwa usanifu na baada ya kukamilika tutaanza kulijenga daraja hilo. Hiyo ndio sababu kubwa ambayo hatukuweka daraja la dharura.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la huo Mto Bubu nadhani nimelijibu pamoja na swali la kwanza kwamba baada ya fedha kupatikana na baada ya usanifu kukamilika, basi hilo daraja litakamilika ili kuunganisha wasafiri kutoka upande wa Kondoa kwenda upande wa Mkoa wa Manyara. Kwa sasa tunawashauri wananchi waendelee kupita kutoka Kondoa kupitia Babati kwenda Katesh na kutoka Sambalang kwenda Babati bila kupita kwenye huo mto. Ahsante. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. SAMWEL X. HHAYUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya Kondoa – Gisambalang – Nangwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Swali la msingi linafanana kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini na changamoto iliyopo Hanang’ inafanana kwa sababu ilikuwa ni wilaya moja. Barabara ya kutoka Mugitu kuja Hydom iliahidiwa na ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi na Mheshimiwa Naibu Waziri aliipita. Je, ni lini tunajengewa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatel Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mugitu - Hydom imeshakamilishwa kufanyiwa usanifu wa kina na sasa hivi kinachosubiriwa ni upatikanaji wa fedha ili ianzwe kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Mbulu kwamba kadri fedha zitakapopatikana barabara hii itajengwa pia na ndio maana tayari usanifu wa kina umeshafanyika ikiwa ni maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)